• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

Posted on: May 19th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya amewataka wananchi waliopata madhara yaliyosababishwa na mvua iliyoambatana na upepo katika Manispaa ya Musoma tarehe 23 Machi, 2025 kutumia misaada wanayopewa kuboresha maisha yao.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi misaada kwa wahanga amewataka kutumia misaada hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuboresha maisha yao baada ya tatizo hilo lililowapata.

“Msaada mtakaopokea leo msiende kutumia ovyo, mtumie kulingana na malengo ya misaada hiyo katika kuboresha maisha yenu baada ya masaibu yaliyowakuta” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya amemshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kutoa fedha na vifaa kama vile mabati, magodogo, mablanketi, ndoo kwa ajili ya waathirika hao.

Aidha, amewashukuru Mbunge wa Viti Maalum Ghati Chomete, Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini Mhe. Vedastus Mathayo, Nyansaho Foundation, mgodi wa Barrick North Mara na wadau wengine waliotoa msaada kwa waathirika hao kwa nyakati tofauti.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Mara Mhe. Juma Chikoka amesema anaishukuru Serikali na wadau wote waliochangia katika maafa hayo na kuwashukuru wananchi kwa ustahimilivu wao wakati Serikali ilipokuwa inatoa msaada kwa makundi mbalimbali kulingana na uathirika wao.

Mhe. Chikoka amewahakikishia wananchi hao kila mmoja aliyeathirika atafikiwa na Serikali na kupewa msaada kulingana na kiasi cha fedha na mali zilizopo.

Mhe. Chikoka amewataka wananchi kuendelea na shughuli zao za maendeleo kwa amani na utulivu wakati huu nchi inapoelekea katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na kuwahakikishia kuwa usalama wakati wote wa uchaguzi.

Kwa upande wake, Mratibu wa Maafa Manispaa ya Musoma Bibi Aines Anderson amesema katika maafa hayo nyumba 196 ziliathirika na kusababisha kaya 139 kukosa makazi na kaya 16 zenye watu 40 zilihifadhiwa katika majengo ya NFRA na kuhudumiwa kwa chakula na malazi kwa siku tatu kabla ya kupewa pesa za pango la miezi sita kwa kila kaya.

Bibi Aines Anderson amesema tangu kutokea kwa maafa hayo, jumla ya nyumba sita za wazee na watu wasiojiweza zimejengwa katika kata za Nyakato, Kitaji, Kwangwa na Rwamlimi na kukarabati nyumba 33 katika kata za Kitaji na Nyakato.  

Amesema msaada unaogawiwa leo ni mabati 568 kwa ajili ya kaya 29, magodoro 91 na mablanketi 100 yaliyotolewa kwa ajili ya kaya 91 na saruji mifuko 70 iliyotolewa kwa ajili ya jengo la kilimo na Shule ya Msingi Mwembeni B zilizoathirika katika tukio hilo.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa