• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara kuanza kutoa huduma Aprili 2020

Posted on: March 6th, 2020

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara ya Kwangwa inatarajia kuanza kutoa huduma katika Jengo la Mama na Mtoto kuanzia tarehe 17 Aprili 2020 baada ya kukamilika ujenzi wa upande huo na huduma zote muhimu za kuwezesha kuanza kufanya kazi.

Hayo yameelezwa leo baada ya kikao cha pamoja kati ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kigoma Malima, wawakilishi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambao ndio wakandarasi na mwakilishi wa Chuo Kikuu cha Ardhi ambaye ni Mshauri Mwelekezi katika mradi huo pamoja na maafisa waandamizi wa serikali.

Akizungumza baada ya kikao hicho Mheshimiwa Lukuvi ameeleza kuwa amewaagiza NHC kuhakikisha kuwa wanafanyakazi ya kukamilisha ujenzi wa hospitali hii kwa usiku na mchana na kuhakikisha kuwa huduma zitaanza kutolewa kwa muda uliopangwa.

 “Kwa sasa Mshauri Mwelekezi anarekebisha michoro ya awali ya majengo hayo ili iweze kukidhi mahitaji yote ya msingi ya majengo ya wakati huu” alisema Mheshimiwa Lukuvi.

Kwa upande wake Mheshimiwa Mwalimu amesema kuwa wanategemea kuwa hospitali hii itaanza kufanyakazi kwa kutoa huduma za mama na mtoto na makubaliano ni kuwa hadi kufikia Julai, 2020 hospitali yote itakuwa imekamilika kutoa huduma kwa wananchi.

“Tunategemea kuwa ujenzi huu ukikamilika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara itahamia hapa Kwangwa na pale ilipo sasa yale majengo yatatumika kama Hospitali ya Manispaa ya Musoma” alisema Mheshimiwa Mwalimu

Aidha amesema kuwa hospitali hii haitakuwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa bali itakuwa ni hospitali ya kibingwa na kibobezi kwa baadhi ya huduma na itatoa huduma kwa wananchi wote wa Kanda ya Ziwa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Adam Kighoma Malima amesema kuwa ziara ya viongozi hawa imesadia sana katika kutatua changamoto zilizokuwa zinaukabili ukamilishaji wa hospitali hii. 

Ujenzi wa Hospitali ya Kwangwa ulianza mwaka 1977 na ulikuwa ukijengwa taratibu hadi mwaka 2018 ambapo Rais wa awamu ya tano Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli alipoamua kutoa shilingi bilioni 15 kwa ajili ya kumalizia ujenzi huu.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa