• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi awataka wakufunzi wa Sensa kuwa mfano

Posted on: July 29th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amewataka wakufunzi wa Sensa ya Watu na Makazi, 2022 kuwafundisha na kuwa mfano mzuri kwa wasimamizi na makarani wa sensa katika Halmashauri zao ili kufanikisha zoezi la Sensa katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 26 Julai, 2022 wakati alipokuwa anafunga mafunzo ya sensa kwa wakufunzi wa sensa ngazi ya Mkoa yaliyofanyika katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare katika Manispaa ya Musoma.

“Serikali imetumia fedha nyingi kugharimia maandalizi ya Sensa hii, ninatambua pia kwa mwaka huu wengi wa makarani sio waajiriwa wa serikali, na hivyo ninaomba mkawafundishe kufanya kazi hii kwa uadilifu na kufuata miiko, taratibu na matakwa ya kazi hii” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha, Mheshimiwa Hapi amewaeleza wakufunzi hao kuwaelekeza wasimamizi na makarani wa sensa kuepuka masuala binafsi, tofauti za kisiasa, itikadi na kidini wakati wa kutekeleza zoezi la Sensa ili kuleta ufanisi wa zoezi hilo.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa sensa ni zoezi muhimu sana kwa Taifa kwa kuwa taarifa zitakazopatikana zitaisaidia serikali katika kupanga mipango ya maendeleo ya wananchi kwa kuzingatia mahitaji halisi.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewataka waratibu wa Sensa kuhakikisha kuwa makarani wa sensa wanapata malipo yao kwa wakati ili kurahisisha utekelezaji wa shughuli za sensa kwa ufanisi.

“Ni vizuri makarani wote na wasimamizi na wahusika wengine wote kwenye zoezi la sensa wapate malipo yao kwa wakati ili kurahisisha utekelezaji wa zoezi la kukusanya taarifa kutoka kwa wananchi kwa ukamilifu” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha, amewaomba Waandishi wa Habari kuendelea kupeleka taarifa za sensa kwa wananchi ili wananchi waweze kupata taarifa sahihi na kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo tarehe 23 Julai, 2022.  

Kwa upande wake, Mratibu wa Sensa Mkoa wa Mara Bwana David Danda ameeleza kuwa mafunzo ya wakufunzi wa sensa ngazi ya Mkoa yamefanyika kwa siku 21 kuanzia tarehe 6 Julai, 2022 na kuwahusisha wakufunzi 296 kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

Bwana Danda ameeleza kuwa mpaka leo wakufunzi hao wamefundishwa, kufanya mitihani na kufuzu mafunzo yao na sasa wapo tayari kwa ajili ya kwenda kuwaelimisha wasimamizi na makarani wa sensa 69,000 ambao wamechaguliwa kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

 Sensa ya Watu na Makazi kwa mwaka 2022 inatarajiwa kufanyika hapa nchini tarehe 23 Agosti, 2022 na kuwahusisha watu wote watakaolala hapa nchini usiku wa kuamkia tarehe 23 Agosti, 2022.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa