• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi atoa wiki mbili VETA kukamilisha kazi

Posted on: June 4th, 2022

HAPI ATOA WIKI MBILI KWA VETA KUKAMILISHA KAZI 

Mkuu Wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amekitaka Chuo cha VETA Mara kukamilisha kazi ya kutengeneza nguzo za majina ya  barabara waliyopewa na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Mkoa wa Mara.

Akizungumza wakati wa kukagua na kujionea utengenezaji wa nguzo hizo, Mheshimiwa Hapi ameridhishwa na ubora wa kazi inayofanywa na Chuo cha VETA Mara na kuwataka kukamilisha kazi hiyo ndani ya wiki mbili.

“Nataka hii kazi iwe imekamilika ndani ya wiki mbili hadi tarehe 19 Juni, 2022 kazi hii iwe imekamilika na nitakuja kukagua kuona kazi ilivyofanyika” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha Mheshimiwa Hapi amekitaka Chuo hicho kuongeza mafundi zaidi katika zoezi la kupaka rangi na kuandika majina ya barabara ili kazi hiyo iweze kukamilika kwa haraka.

“Mkiona inafaa mnaweza kuwatumia wanafunzi wa Sekondari ya Ufundi Musoma wanaosomea masuala ya rangi wakawasaidia na ikawa kama sehemu yao ya mafunzo kwa vitendo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuendelea kuwahamasisha wananchi kuweka nguzo na majina ya mitaa yao ili iweze kutambulika kwa urahisi.

Kwa upande wake Meneja wa TARURA Mkoa wa Mara Mhandisi Boniface William ameeleza kuwa TARURA imewapa VETA kazi ya kutengeneza nguzo 5892 za barabara za TARURA kwa gharama ya shilingi milioni 206.

Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa Mhandisi William ameeleza kuwa vifaa vya mradi huo vimenunuliwa na TARURA kwa gharama ya shilingi zaidi ya milioni 500.

“Hii kazi imeletwa VETA kwa sababu tuliamini VETA wataifanya kwa ubora na viwango vinavyotakiwa katika kufanikisha operesheni hii ya anuani za makazi” alisema Mhandisi William.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Chuo cha VETA Mara Mwalimu David Louis ameeleza kuwa kwa mujibu wa mkataba kazi hiyo ilitolewa tarehe 13 Mei, 2022 na ilipaswa kukamilika tarehe 13 Juni, 2022.

“Kwa sasa kazi ya ukataji wa mabomba na utengenezaji wa vibao imekamilika na kazi ya kupaka rangi na kuandika majina imeanza na inaendelea” alisema Mwalimu Louis

Mwalimu Louis ameeleza kuwa katika kutekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa wataongeza mafundi na vibarua ili kuharakisha zoezi hilo.

Utengenezaji wa nguzo za majina ya barabara ni sehemu ya utekelezaji wa Operesheni ya Anuani za Makazi ambayo imefanyika hapa nchini na kufikia mwisho tarehe 30 Mei, 2022.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa