• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi atoa wiki mbili kukamilisha miradi

Posted on: July 15th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameiagiza Sekretariati ya Mkoa wa Mara kukamilisha miradi mine ya ujenzi na ukarabati wa nyumba za viongozi wa huu inayotekelezwa katika Manispaa ya Musoma.

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo hayo leo tarehe 14 Julai 2021 katika ziara yake aliyoifanya kukagua miradi mine inayotelekelezwa kwa mfumo wa force account na kusimamiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara katika Manispaa ya Musoma.

“Ninatoa wiki mbili miradi hii minne yote iwe imekamilika…..ninataka ofisi yangu iwe ni ofisi ya mfano katika utekelezaji wa miradi ya serikali katika Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Hapi.

Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo, Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi, usimamizi na ugawaji wa kazi kwa mafundi wa miradi hiyo ambao wanaajiri mafundi wengine katika utekelezaji na hivyo kuchelewesha utekelezaji wa miradi hiyo.

Aidha Mkuu wa Mkoa ameagiza kupatiwa taarifa ya kina kuhusu matumizi ya fedha na hususan fedha zilizotumika katika manunuzi ya vifaa na kulipa mafundi katika miradi hiyo.  

Awali akitoa taarifa ya miradi hiyo Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Miundombinu Mhandisi Faustin Tarai ameeleza kuwa miradi hiyo ilianza kutekelezwa kuanzia tarehe 15 Machi 2021 na inatarajiwa kukamilika tarehe 19 Julai 2021.

Aidha Bwana Tarai ameeleza kuwa kuwa vifaa vyote kwa ajili ya miradi hiyo vilishanunuliwa na malipo ya mafundi yanaendelea kutolewa kulingana na madai wanayoyatoa baada ya kukamilisha sehemu ya kazi.

Katika kukagua miradi hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela; Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mheshimiwa Alfany Haule, Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Sekretariati ya Mkoa, wataalamu wa ofisi ya Katibu Tawala Wilaya ya Musoma pamoja na waandishi wa habari.

Miradi inayotekelezwa na Sekretariati ya Mkoa wa Mara katika Manispaa ya Musoma ni pamoja na  ujenzi wa nyumba ya Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Afya; ujenzi wa nyumba ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Musoma; ukarabati wa nyumba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara;  na ukarabati wa nyumba ya Mkuu wa Wilaya ya Musoma ambayo imefikia katika hatua tofauti za ukamilishaji wake.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa