• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi ataka kasi ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

Posted on: August 16th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amewataka viongozi, watendaji na mkandarasi wa mradi wa ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kuongeza kazi katika utekelezaji wa mradi huo.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 15 Agosti 2021 wakati alipofanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kukagua miradi ya maendeleo.

“Haiwezekani fedha zimeletwa hapa miezi mitano iliyopita hadi leo bado mpo kwenye hatua ya kuchimba mashimo ya nguzo ya jengo hili, uzembe huu haukubaliki kabisa, sio kwa wakati wangu” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ametoa miezi minne jengo hilo liwe limekamilika huku akimwagiza mkandarasi wa mradi huo, SUMA JKT kuongeza vibarua na mafundi na kutekeleza mradi huo usiku na mchana.

Mkuu wa Mkoa pia ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kufanya uchunguzi kwa nini vifaa vya mradi huo havijanunuliwa viwandani moja kwa moja na badala yake vimenunuliwa katika maduka na kwa mawakala.

Mheshimiwa Hapi amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kufuatilia matumizi ya shilingi milioni 37 zinazodaiwa zimetumika kununua nguzo, nyaya na vifaa vya umeme unaokuja kwenye mradi huo kuona uhalali wake.

Wakati huo huo, Mheshimiwa Hapi ametoa siku saba kwa Wakala wa Maji Mijini na Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Bunda kuhakikisha mradi wa maji wa Iramba unaokarabatiwa uliotumia fedha zaidi ya shilingi milioni 473 unatoa maji kwa wananchi.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo baada ya kutokuridhishwa na maelezo ya RUWASA waliyoyatoa na hali halisi ya ukarabati wa mradi huo.

Mradi huo ulizinduliwa Januari 1978 na ukaharibika mwaka 2005 na serikali ikaleta fedha za kuukarabati shilingi milioni 500 tangu 2019 na mpaka sasa bado hautoi huduma ya maji kwa wananchi. 

Katika siku ya kwanza ya ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Mheshimiwa Hapi ametembelea miradi miwili ya ujenzi wa barabara katika eneo la Iramba na Nyamswa, mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi za halmashauri katika eneo la Kibara, mradi wa maji katika eneo la Iramba.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa ameambatana na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara Mheshimiwa Samweli Kiboye, Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mheshimiwa Joshua Nassari na viongozi pamoja na watendaji wengine wa chama na serikali.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi aipongeza Bunda TC kwa hati safi miaka mitano mfululizo

    June 13, 2025
  • Mtambi aitaka Bunda DC kuwasilisha Mkakati wa kukusanya milioni 700

    June 13, 2025
  • Mtambi aipongeza Halmashauri ya Rorya

    June 12, 2025
  • Mtambi awataka wanawake kugombea nafasi za uongozi

    June 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa