• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi akitaka Chuo cha Ugaga Musoma kujiimarisha

Posted on: August 6th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amekitaka Chuo cha Uganga Musoma (Musoma COTC) kujiimarisha kwa kuanza kukarabati na kuongeza miundombinu kwa kutumia mapato ya ndani.

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo hayo leo tarehe 2 Agosti 2021 wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Manispaa ya Musoma.

“Kwa kutumia mapato ya ndani mnauwezo wa kuanza kukarabati chuo hiki hata jengo moja moja na kuanza kujenga majengo mengine pia” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha amekitaka kupanuka kwa kutafuta eneo kubwa ili kiweze kukua zaidi na kuchukua wanachuo wengi zaidi kwa manufaa ya taifa.

Mheshimiwa Hapi amesema kuwa Chuo hicho kinapaswa kuchangamkia fursa ya mpango wa kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere cha Kilimo, Sayansi na Teknolojia ambapo kikikamilika kinatarajiwa kuwa na kampasi yake katika Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.

“Hapo zitatolewa kozi za fani mbalimbali za afya ya binadamu, mkikitumia vizuri mtapata wahadhiri, sehemu ya wanachuo wenu kufanya mazoezi ya vitendo na wataalamu wengineo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Amekipongeza Chuo hicho kwa kufundisha vizuri wanachuo pamoja na upungufu wa watumishi uliopo katika Chuo hicho.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo hicho Dkt. Ibrahim A. Bakari ameeleza kuwa Chuo hicho kwa sasa kina upungufu mkubwa wa wafanyakazi.

“Kwa sasa Chuo kina wafanyakazi 12 na kina upungufu wa wafanyakazi 37 na kati ya wafanyakazi waliopo wakufunzi ni saba tu ikilinganishwa na mahitaji ya wakufunzi 25 kulingana na idadi ya wanafunzi” alisema Dkt. Bakari.

Dkt. Bakari ameeleza kuwa ili kukabiliana na tatizo la upungufu wa wafanyakazi wamekuwa wakiwatumia zaidi wafanyakazi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara pamoja na vituo vingine vya kutolea huduma za afya vilivyopo katika Mkoa wa Mara.

Aidha ameeleza kuwa Chuo hicho kimefanikiwa kuongeza makusanyo baada ya jitihada za kuongeza wanafunzi lakini kwa sasa wanakabiliwa na changamoto ya upungufu na uchakavu wa miundombinu.

Mheshimiwa Hapi akiwa chuoni hapo pamoja na ujumbe alioambatana nao alikagua mazingira, akazungumza na wanachuo na watumishi wa Chuo hicho.

Chuo cha Uganga Musoma kilianzishwa miaka ya 1970 na miundombinu yake mingi ilijengwa wakati huo na kinatoa Stashahada za Uuguzi na Udaktari pamoja na Astashahada ya Udaktari.

Mheshimiwa Hapi aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dkt. Alfany Haule, watumishi wa Manispaa ya Musoma.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa hapi alitembelea Kiwanda cha Samaki cha Alpha, Shule ya Sekondari ya Mara, Shule ya Msingi Kigera A, Kituo cha Afya Mshikamano na mradi wa ukarabati wa Uwanja wa Ndege wa Musoma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi aipongeza Bunda TC kwa hati safi miaka mitano mfululizo

    June 13, 2025
  • Mtambi aitaka Bunda DC kuwasilisha Mkakati wa kukusanya milioni 700

    June 13, 2025
  • Mtambi aipongeza Halmashauri ya Rorya

    June 12, 2025
  • Mtambi awataka wanawake kugombea nafasi za uongozi

    June 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa