• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi akagua maandalizi ya kutekeleza miradi

Posted on: November 5th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ametembelea Wilaya ya Rorya na Tarime kukagua maandalizi ya ujenzi wa miradi ya madarasa na vituo vya afya vilivyotengewa fedha na serikali.

Mheshimiwa Hapi ametembelea maeneo hayo leo tarehe 16 Oktoba 2021 na kutoa maelekezo kwa viongozi kuhusiana na maandalizi hayo.

“Lengo la ziara hiii ni kuangalia maeneo ambapo miradi hii itajengwa pamoja na kukagua maandalizi ya kuanza kwa miradi hii mara baada ya fedha kuruhusiwa kuanza kutumika.

Mheshimiwa Hapi alitembelea mradi wa upanuzi wa zahanati kuwa Kituo cha Afya Nyamagaro na ujenzi wa Madarasa katika Shule ya Sekondari ya Nyamtinga katika Wilaya ya Rorya.

Aidha akiwa katika Wilaya ya Tarime, Mheshimiwa Hapi alitembelea mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya katika eneo la Kitenga katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na mradi wa ujenzi wa madarasa katika Shule ya Sekondari ya Nkende katika Halmashauri ya Mji wa Tarime. 

Akizungumza na wakati akitembelea miradi hiyo Mheshimiwa Hapi amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuendelea na maandalizi ya ujenzi huo pamoja na kuunda kamati za ujenzi huo mapema iwezekanavyo.

Aidha Mheshimiwa Hapi amevielekeza vyombo vya ulinzi na usalama kufuatilia miradi hiyo ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua watu wote watakaohusika na ubadhilifu wa aina yoyote ile katika miradi hiyo.

Mheshimiwa Hapi amemuagiza Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) kuhakikisha barabara ya kuingia katika Shule ya Sekondari Mtinge inapitika muda wote.

Aidha amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha maeneo ambayo miradi hii inaenda kujenga hayana migorogo na wananchi.

“Serikali haina fedha za kuanza kulipa watu fidia, kama maeneo yaliyoainishwa katika miradi hii yana mgogoro, leteni mapendekezo ya kupeleka miradi hiyo maeneo mengine haraka iwezekanavyo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka watendaji wote watakaohusika katika utekelezaji wa miradi hiyo kutimiza wajibu wao kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma za kijamii zinazokusudiwa kutoaka na miradi hiyo.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa pia alipata nafasi ya kuzungumza na wananchi wa eneo la Nyamagaro katika Wilaya ya Rorya na maeneo ya Kitenga na Nkende katika Wilaya ya Tarime.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa aliambatana na Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Wilaya, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa, Mwakilishi wa Afisa Elimu wa Mkoa, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri na watendaji wengine.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa