• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi aitaka Shule ya Sekondari ya Ufundi Musoma ijiongeze

Posted on: November 29th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameitaka Shule ya Sekondari ya Ufundi ya Musoma itumie uwezo iliyonayo ili kujiongezea mapato yanayotokana na kazi za ufundi wa kutengeneza bidhaa mbalimbali.

Mheshimiwa Hapi ametoa kauli hiyo leo tarehe 23 Novemba 2021 wakati alipokuwa katika ziara ya kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa, utengenezaji wa matofali pamoja na utengenezaji wa viti na meza kwa ajili ya vyumba vya madarasa katika Wilaya ya Musoma.

“Kwa mashine, wataalamu na nguvu kazi iliyopo hapa, mnauwezo wa kutengeneza viti, meza, vitanda, milango, madirisha, magari na kadhalika mkaviuza kwa bei ya soko ili kuongeza mapato ya Shule na utaalamu wa vitendo kwa wanafunzi na walimu pia” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza viti na meza vinavyotengenezwa vinaubora na gharama yake ni nafuu ikilinganishwa na ubora uliopo mitaani na kuwataka waongeze uzalishaji ili kiwe kituo cha kununua mahitaji kwa taasisi na watu binafsi.

Aidha Mheshimiwa Hapi amewataka wanafunzi wanaosoma masomo ya ufundi kufanyakazi kwa bidii ili waweze kupata elimu, ujuzi na uzoefu kwa vitendo katika kuunda na  kutengeneza vitu mbalimbali.

Mkuu wa Mkoa ambaye pia ni Mlezi wa Shule hiyo, ameipongeza shule hiyo kwa kutekeleza kwa haraka maagizo aliyoyatoa awali kuhusu kufufua mashine zilizopo katika shule hiyo ili kuweza kupata kazi mbalimbali.

Aidha ameipongeza Shule hiyo kwa kupiga hatua katika mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa na kuwa mfano katika Manispaa ya Musoma ambapo ujenzi wa boma umeshakamilika na wanatarajia kuanza kuezeka.

Awali akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Ufundi Musoma Mwalimu Mohamed Kajeri ameeleza kuwa kwa sasa Shule hiyo imepokea oda ya kutengeneza viti na meza kutoka katika Halmashauri tano za Mkoa wa Mara.

Mwalimu Kajeri ameeleza kuwa kutokana na mpangokazi wao walivyojipanga, wanatarajia kukamilisha kutengeneza viti na meza hizo ndani ya wiki mbili na tayari vifaa vilikuwa vimeshanunuliwa msafara ulishuhudia mbao na vyuma vikiwa vinashushwa shuleni hapo.

Aidha Mwalimu Kajeri Amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuwapa wazo la kuanza kujitegemea bidhaa mbalimbali kwa kutumia wataalamu na vifaa vilivyopo na kwa sasa wanapata wateja hususan kutoka katika taasisi za umma.  

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa pia ametembelea mradi wa ujenzi wa madarasa matatu na ofisi moja katika Shule ya Sekondari Mugango, mradi wa kufyatua matofari wa Kikosi cha Jeshi Makoko katika eneo la Bukima katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Mheshimiwa Hapi pia ametembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika Shule ya Sekondari ya Nyasho, mradi wa ujenzi wa vyumba viwili na ofisi moja na karakana ya kutengeneza bidhaa mbalimbali katika Shule ya Sekondari ya Ufundi Musoma katika Manispaa ya Musoma.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Musoma, viongozi wa Chama cha Mapinduzi, Wakurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na Manispaa ya Musoma, wakuu wa idara na watendaji wengine.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa