• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi aitaka MMG kutekeleza maagizo ya Serikali

Posted on: July 22nd, 2022

HAPI AITAKA MMG KUTEKELEZA MAAGIZO YA SERIKALI

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameutaka Mgodi wa Dhahabu wa MMG Limited kutekeleza maagizo ya serikali yanayotolewa kwa mujibu wa sheria mbalimbali zinazosimamia sekta ya madini hapa nchini.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 19 Julai, 2022 wakati alipoutembelea mgodi huo uliopo katika Kijiji cha Seka, katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na kuutaka kutoa maelezo ya kukiuka maagizo yake aliyotoa awali.

“Ninataka mgodi utoe maelezo kwa nini haujatekeleza maagizo yangu na maagizo ya ofisi ya madini Mkoa wa Mara kuhusu kulipa ushuru wa huduma, kuwa na mpango wa uwajibikaji kwa jamii (CSR) na kuwa na Meneja Mkuu wa Kampuni” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa ushuru wa huduma na CSR sio msaada, ni masuala ya kisheria lazima yatekelezwe na wawekezaji wote hapa nchini kwa ajili ya maendeleo ya Halmashauri hiyo.

Wakati huo huo, Mheshimiwa hapi ameuagiza mgodi huo kuandaa mpango wa kufunga mgodi huo kwa mujibu wa sheria na kuutaka mgodi huo kuwasilisha majina ya kampuni, thamani ya zabuni walizopewa na muda wa utekelezaji ili wazabuni hao waweze kulipa ushuru wa huduma na CSR kwa Halmashauri.

Mheshimiwa Hapi pia ameushauri mgodi huo kujenga uzio kuzunguka eneo lake ili kuzuia uhalifu unaoweza kujitokeza kwa kuwa hauna uzio katika sehemu kubwa ya mgodi huo.

Mheshimiwa Hapi ameutaka mgodi huo kumlipa Bibi Sharma Mwanyoka mjasiriamali ambaye alikuwa anafanya biashara na mgodi huo ambaye anadai shilingi milioni 5 kuanzia mwaka 2018.

Aidha, ameutaka mgodi huo kuajiri Afisa Uhusiano ili kuweka mahusiano mazuri na wananchi wanauzunguka mgodi huo na kuachana na mfumo wa sasa ambapo Meneja wa Utawala ndiye Mhasibu, mtu wa utawala na Afisa Uhusiano mtu mmoja.

Kwa upande wake, Afisa Madini Mkoa wa Mara Mhandisi Joseph Kumburu ameeleza kuwa katika ukaguzi wa wataalamu wa madini katika mgodi huo, waliagiza mgodi huo kumteua Meneja Mkuu ambaye kwa mujibu wa Sheria za Madini ndiye mtu wa kuzungumza na serikali.

“Kwa sasa, hawana mtu mwenye cheo hicho na kila wakiitwa kwa jambo fulani wanamleta afisa tofauti kwenda kusilikiliza na tuliwapa muda wa siku 30 zimeshaisha lakini suala hilo halijatekelezwa” alisema Mhandisi Kumburu.

Aidha, Mhandisi Kumburu ameeleza kuwa mgodi ulikuwa umeelekezwa kununua mavazi zaidi ya usalama (PPE) kwa ajili ya wafanyakazi lakini hawajatekeleza.

Bwana Kumburu ameeleza kuwa mgodi huo uliagiza pia kumwaga maji katika barabara zake ili kupunguza vumbi kwa wananchi wanaouzunguka mgodi huo ambalo halijatekelezwa.

  Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa, kamati ya usalama ya Mkoa, Wilaya ya Musoma na baadhi ya watumishi kutoka ofisi ya madini, ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa