• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi aagiza uchunguzi Sekondari mpya ya Binagi

Posted on: July 22nd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 13 Julai, 2022 amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kuunda tume ya uchunguzi kuhusu ujenzi wa Shule ya Sekondari ya katika Kata ya Binagi na kuwasilisha taarifa ndani ya wiki mbili.

Akizungumza katika kikao maalum cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa amepata taarifa kuwa fedha zilizoletwa kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo zimeisha na ujenzi haujakamilika.

“Serikali ilileta fedha kwa kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya kata katika Kata ya Binagi na taarifa nilizonazo fedha zimeisha, ujenzi umesimama na haujakamilika, ninataka taarifa ndani ya wiki mbili” alisema Mheshimiwa Hapi.

Fedha za ujenzi wa Shule ya Binagi zinatokana na fedha za tozo ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ilipata fedha za kujenga shule mbili mpya katika Kata ya Binagi na Kata ya Sirari.

Aidha, Mheshimiwa Hapi amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa kuhakikisha inaongeza watumishi katika Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ili kuimarisha utendaji katika kitengo hicho.

“Halmashauri hii ina fedha nyingi na miradi mingi ya maendeleo haitakiwi kuwa na Mkaguzi wa Ndani mmoja tu ambaye pia ndiye Mkuu wa Kitengo, hii inasababisha mapungufu zaidi kwenye usimamizi wa fedha na miradi ya Halmashauri” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka madiwani wa Halmashauri hiyo kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhakikisha wataalamu hususan wahandisi wanafika katika miradi inayotekelezwa katika maeneo yao.

Katika kikao hicho pia Mheshimiwa Hapi alitoa mrejesho wa maamuzi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.) kuhusiana na matumizi ya fedha za CSR zinazotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara kwa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bwana Solomon Shati ameeleza kuwa Halmashauri  ya Wilaya ya Tarime imepata hati safi na kwa kipindi cha miaka sita mfululizo kuanzia mwaka wa fedha 2015/2016 hadi 2020/2021.

Hata hivyo Bwana Shati ameeleza kuwa Halmashauri ilikuwa na jumla ya hoja 98 na kati ya hoja hizo hoja za miaka ya nyuma 60 na hoja 38 ni za mwaka wa fedha 2020/2021 na maagizo mawili ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC).

Bwana Shati ameeleza kuwa katika hoja zilizopita 60 za miaka ya nyuma, hoja 34 zimeshatekelezwa na kufungwa, hoja 18 zipo kwenye hatua mbalimbali za utekelezaji, hoja 02 zimejirudia huku hoja 06 hazijatekelezwa.

Aidha, Bwana Shati ameeleza kuwa kati ya hoja 38 mpya hoja 19 zimefungwa hoja 18 zipo kwenye utekelezaji na hoja moja ni hoja za kujirudia na kwamba Halmashauri hiyo imefanikiwa kufunga asilimia 54 ya hoja zote zilizotolewa na CAG.

 Kikao cha Baraza la Madiwani Maalum kilihudhuriwa pia na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Kamati ya Ulinzi ya Mkoa na Wilaya ya Tarime, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa, Katibu Tawala wa Wilaya na viongozi wengine.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa