• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Tumieni magari haya kutatua kero za wananchi- Mtambi

Posted on: May 22nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo tarehe 22 Mei, 2025 amekabidhi magari mapya yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan yenye thamani ya shilingi milioni 504 kwa ajili ya Wakuu wa Wilaya za Tarime na Musoma.

Akizungumza wakati wa kukabidhi magari hayo kwa Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka na Mkuu wa Wilaya ya Tarime Meja Edward Gowelle, Mhe. Mtambi amewataka Wakuu wa Wilaya kutumia magari hayo kutatua kero za wananchi katika maeneo yao.

“Tumieni magari haya kuwatembelea wananchi kwa lengo la kusikiliza na kutatua kero za wananchi, kwa sasa hamna kisingizio cha kushindwa kufika sehemu yoyote kwa kuwa haya magari yanapita mahari popote hata ambapo hamna barabara nzuri haya yanapita” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema baada ya Mhe. Rais kutoa magari hayo amemaliza changamoto ya usafiri kwa Wakuu wa Wilaya ambapo awali magari kwa baadhi ya Wakuu wa Wilaya yalikuwa yanazimwa kutoka katika taasisi nyingine za umma lakini kwa sasa Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa Mara wanayo magari mapya waliyonunuliwa na Mhe. Rais.

Mhe. Mtambi amewataka Wakuu wa Wilaya kuyatunza magari hayo na kuhakikisha wanasimamia madereva wanayoyaendesha magari hayo ili waweze kuchukua tahadhari katika uendeshaji wao na kufuatilia ratiba za matengenezo ya kawaida ya magari hayo.

Kanali Mtambi ametumia fursa hiyo na kuwataka Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Mara kutumia magari hayo kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 ili waweze kuchagua viongozi bora wanaopenda maendeleo.  

Akizungumza katika hafla ya mapokezi ya gari hizo, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Meja Edward Gowelle ameishukuru Serikali kwa kupatiwa magari ambayo yatawawezesha kufika katika maeneo yao ya utawala kwa haraka na kuwahudumia wananchi.

“Haya magari yatatusaidia sana kuwafikia wananchi na kusikiliza na kutatua kero zao, kukagua miradi ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa katika Wilaya zetu na yataongeza kasi yetu katika kuwahudumia wananchi” amesema Mhe. Gowelle.

Mhe. Gowelle ameahidi kuwa watayatumia magari hayo kama yalivyokusudiwa na watasimamia kuhakikisha yanatunzwa na kutumika kwa shughuli za Serikali katika kuwahudumia wananchi na kuahidi kuyatunza ili yaweze kudumu muda mrefu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka watatekeleza maagizo yote ya Mkuu wa Mkoa na kuhakikisha magari hayo yanaleta tija kwa wananchi.

“Tunashukuru sana kwa kupatiwa magari haya ambayo yatatusaidia kufuatilia utekelezaji wa miradi na kutatua kusikiliza kero za wananchi kwa wakati” amesema Mhe. Chikoka.  

Hafla ya kukabidhi magari hayo imehudhuliwa na Wakuu wa Wilaya, watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala wa Wilaya na baadhi ya watumishi kutoka Ofisi za Wakuu wa Wilaya waliopokea magari hayo.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Tumieni magari haya kutatua kero za wananchi- Mtambi

    May 22, 2025
  • CCM yapongeza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Mara

    May 20, 2025
  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.