• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Units
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi aipongeza Manispaa ya musoma kwa hati safi miaka mitano mfululizo

Posted on: June 11th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi ameshiriki Baraza Maalum la Madiwani linalojadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali katika Manispaa ya Musoma na kuipongeza Manispaa hiyo kwa kupata hati safi kwa miaka mitano mfululizo.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtambi amelipongeza Baraza la Madiwani, Menejimenti, watumishi wa Manispaa hiyo na wadau wote waliohusika katika kuiwezesha Manispaa kupata hati safi ya ukaguzi.

“Hii inaonyesha Manispaa ina uimara wa mifumo ya usimamizi wa mapato na matumizi ya Manispaa na juhudi za kila mmoja katika utekelezaji wa majukumu” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amelitaka Baraza la Madiwani kusimamia kasoro za usimamizi wa mikataba na manunuzi ili thamani ya fedha katika miradi iweze kuonekana na kuhakikisha manunuzi yote yanafanyika kupitia mfumo wa ununuzi na kupunguza hoja za ukaguzi katika Manispaa hiyo. 

Kanali Mtambi ameiagiza Halmashauri ya Manispaa ya Musoma kuandaa mkakati wa kumaliza hoja za ukaguzi na maagizo ya LAAC na kuuwasilisha ofisini kwake tarehe 30 Juni, 2025 na kuhakikisha maafisa wanaosababisha hoja wanachukuliwa hatua za kiutumishi.

Mhe. Mtambi ametoa wiki mbili kwa Katibu Tawala Mkoa wa Mara kumrejesha Bashiri Gasori aliyekuwa Afisa Uvuvi wa Manispaa hiyo na baadaye kuhamia Manispaa ya Ilemela baada ya kubainika kuwa uhamisho wake haukuwa halali.

Mhe. Mtambi amesema hali ya ukusanyaji wa mapato katika Manispaa ya Musoma hairidhishi na kuitaka kuweka mikakati ya kuongeza vyanzo vya mapato na kukusanya mapato kwa ufanisi ili kupata fedha za kuiendesha Halmashauri na kutekeleza miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka amesema hoja nyingi za Halmashauri hiyo zilipaswa kuwa zimefungwa kwa sababu majibu ya hoja nyingi kati ya hizo yapo wazi na ndani ya uwezo wa Manispaa kujibu.

Mhe. Chikoka amesema Manispaa hiyo itaandaa utaratibu wa kuwatambua ni maafisa gani wanaowasababishia hoja za ukaguzi watawachukulia hatua na kuwataka watumishi kila mtu atimize wajibu wake. 

Mhe. Chikoka amesema Wilaya ya Musoma itasimamia uandaaji wa mkakati wa kukamilisha hoja za ukaguzi na itahakikisha Manispaa inawasilisha mkakati huo kabla ya tarehe 30 Juni, 2025 na inafunga hoja nyingi ambazo majibu yake yamo ndani ya uwezo wa Manispaa. 

Kwa upande wake, Mwekahazina wa Manispaa ya Musoma ACPA Emmanuel Abraham amesema katika mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ilikuwa na hoja 72 na baada ya uhakiki hoja 37 zimefungwa huku hoja nyingine 48 zikiendelea kufayiwa kazi.

Aidha, Bwana Abraham amesema Manispaa ilikuwa na maagizo saba ya Kamati ya Bunge ya Fedha za Serikali za Mitaa (LAAC) ambapo maagizo mawili yamefungwa na maagizo matano yanaendelea kufanyiwa kazi.

Bwana Abraham amesema pamoja na HAlmashauri hiyo kupata changamoto ya kufunga hesabu katika mfumo wa uhasibu serikalini (MUSE) lakini baada ya hesabu hizo kufungwa imepata hati safi ya ukaguzi.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Musoma, Maafisa kutoka ofisi za ukaguzi na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, madiwani na menejimenti ya Manispaa ya Musoma.

Announcements

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • View All

Latest News

  • Mwenge wa Uhuru Wapitisha miradi 68 ya bilioni 26.5 Mara

    August 23, 2025
  • RC Mtambi akutana na viongozi wa dini na kuwasistiza kuhamasisha amani

    August 22, 2025
  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.