• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Units
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mita mpya kupunguza malalamiko ya bili za maji- BUWSSA

Posted on: July 4th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Bunda (BUWSSA) Bi. Esther Gilyoma amezitambulisha mita mpya ya maji ambazo zitaanza kufungwa katika Mji wa Bunda hivi karibuni zitakazomwezesha mteja kulipia huduma za maji kabla ya kutumia zitasaidia katika kupunguza malalamiko ya kulipia bili za maji.

“Mamlaka imekuwa ikipokea malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu bili za maji na sasa tumepata mwarubaini utakaomaliza kero hii kwa kuwawezesha wananchi kulipia maji kabla ya kuyatumia kulingana na uwezo wao” amesema Bibi Gilyoma.

Akizungumza katika hafla ya mapokezi ya mita hizo, Bi. Gilyoma amesema mita hizo zitatumika katika maeneo yote yenye mtandao wa maji wa mamlaka hiyo baada ya wananchi kuchangia gharama za kufungiwa mita hizo.

Bi. Gilyoma amezitaja faida za mita hizo kuwa ni pamoja na kupunguza malalamiko ya wateja kulimbikiziwa bili, kumwezesha mteja kupanga matumizi yake ya maji kulingana na kipato chake, kumwondolea mwenye nyumba kero ya kulipa bili ya maji iliyotumiwa na wapangaji baada ya wao kuondoka.

Bi. Gilyoma amewahamasisha wananchi na hususan wenye nyumba zenye wapangaji, taasisi na maeneo ya biashara kuchangamkia kuzinunua mita hizo ili kuwawezesha kupunguza migogoro isiyo ya lazima na BUWSSA na wapangaji wao kutokana na bili za maji. 

Mkurugenzi Mtendaji huyo amesema kwa sasa upatikanaji wa maji katika Mji wa Bunda na maeneo yanayohudumiwa na mamlaka hiyo upo kwa asilimia 85 na kwa sasa Mamlaka hiyo inao wateja zaidi ya 10,000.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Wazo PIC Technology Limited Bwana Yoweri Maximilian Chacha amesema Kampuni hiyo ni msambazaji wa mita hizo kwa miaka mitatu sasa na imezisambaza katika Mamlaka mbalimbali za maji katika Mikoa ya Mara, Mtwara na Simiyu.

“Mita hizi zina ubora wa hali ya juu na zimepata ithibaki kitaifa na kimataifa na tangu tumeanza kuzifungwa kwa miaka mitatu hatujapata malalamiko kutoka kwa wateja na mamlaka za maji kuhusiana na ubora” amesema Bwana Chacha.

Bwana Chacha amesema mtumiaji wa mita hiyo ataitumia kama ilivyo mita za umeme wa luku kwa kununua token na kuchaji ili kupata huduma za maji kulingana na malipo yaliyofanyika.  

Hafla ya mapokezi ya mita hizo zaidi ya 1,000 zitakazofungwa katika Mji wa Bunda imehudhuriwa na watumishi wa BUWSSA na kampuni ya Wazo PIC Technology Limited inayohusika na usambazaji wa mita hizo hapa nchini.

Announcements

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • View All

Latest News

  • Mwenge wa Uhuru Wapitisha miradi 68 ya bilioni 26.5 Mara

    August 23, 2025
  • RC Mtambi akutana na viongozi wa dini na kuwasistiza kuhamasisha amani

    August 22, 2025
  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.