• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Units
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Miradi ya TACTIC kuboresha muonekano wa Musoma

Posted on: August 12th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 12 Agosti 2025 amekuwa mgeni rasmi katika hafla ya utiaji saini ujenzi wa Miradi ya Uboreshaji wa Miji Tanzania (TACTIC) katika Manispaa ya Musoma itakayogharimu shilingi bilioni 19.975.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mtambi amesema miradi hiyo inayotekelezwa katika Miji 45 hapa nchini inadhaminiwa na Benki ya Dunia na itakapokamilika itabadilisha  mandhari ya Manispaa ya Musoma.

“Binafsi nina furaha kubwa, maana ujenzi wa miradi hii ikiwamo Soko la Nyasho, barabara za ndani ya Manispaa na Stendi ya Bweri itasadia kubadilisha muonekano wa Manispaa ya Musoma” amesema Kanali Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema miradi hii itakapokamilika italeta mabadiliko chanya kwa wananchi na wageni katika Manispaa ya Musoma na kuboresha mazingira ya biashara na kupandisha thamani ya maeneo husika itapanda na kuongeza mapato ya Manispaa ya Musoma.

Mhe. Mtambi amewataka viongozi na wataalamu kuisimamia vizuri miradi hiyo ili iweze kukamilika kwa wakati na kwa ubora na kumtaka mkandarasi wa miradi hiyo MS Henan Highway Engineering Group Company Limited kutekeleza mradi huo kwa ubora na kwa wakati kulingana na mkataba.

Awali akitoa taarifa ya mradi huo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma Ndugu Bosco Nduguru amesema mradi hiyo inatarajiwa kutekelezwa kwa muda wa miezi 15 kuanzia tarehe 15 Agosti, 2025 hadi Novemba, 2026 na itahusisha ujenzi wa miradi mikubwa mitatu pamoja na ofisi za usimamizi na uratibu wa ujenzi wa miradi hiyo.

Ndugu Ndunguru amesema miradi itakayojengwa katika Manispaa ya Musoma kupitia mradi wa TACTIC ni pamoja na barabara tatu za Mukendo, Shaabani na Musoma Bus –Saanane; Soko la Nyasho na Stendi ya Bweri.   

Hafla hiyo imehudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia miundombinu kutoka Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Musoma, viongozi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara, watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Halmashauri ya Manispaa ya Musoma na Mkandarasi wa miradi hiyo. 

Announcements

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • View All

Latest News

  • Mwenge wa Uhuru Wapitisha miradi 68 ya bilioni 26.5 Mara

    August 23, 2025
  • RC Mtambi akutana na viongozi wa dini na kuwasistiza kuhamasisha amani

    August 22, 2025
  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.