• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Malima ataka wazazi wawalinde watoto na Corona

Posted on: May 6th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amewataka wazazi wa Mkoa wa Mara kuwalinda watoto wao dhidi ya homa ya mapafu inayosababishwa na virusi ya Corona maarufu kama COVID 19.

Mheshimiwa Malima ametoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na wananchi wa eneo la Nyamongo katika Wilaya ya Tarime kuhusiana na malipo ya fidia ya maeneo yao yatakayochukuliwa na Mgodi wa Barrick North Mara.

“Serikali haijafunga shule na vyuo ili watoto watembee ovyo mitaani na kushiriki shughuli zinazowahatarisha  na maambukizi ya Corona, serikali ilitaka wazazi wawalinde watoto wao na ikiwezekana wakae nyumbani” alisema Malima.

Ameeleza kuwa kwa sasa wanafunzi hawapo likizo ya kawaida na wanatakiwa wakae ndani ili waweze kulindwa na sio kuachiwa wanatembea ovyo na kufanyishwa shughuli katika maeneo hatarishi hususan kwenye mikusanyiko ya watu.

Aidha amewapongeza wananchi hao kwa kuchukua tahadhari ya Corona kwa kukaa mbalimbali katika mkutano huo jambo ambalo amesema linauwezo wa kuwaepusha watu na Corona.

Amewataka kutoa taarifa za wageni wanaoingia katika maeneo yao hususan kutoka nchi jirani ya Kenya bila kufuata utaratibu ili waweze kudhibitiwa na hivyo kudhibiti ugonjwa huo kuingia Mkoa wa Mara.

Amewataarifu kuwa kwa sasa shughuli zote za misiba zitafanywa na watu wachache na ndani ya muda mfupi ili kuweza kuwakinga watu dhidi ya maambukizi ya Corona aidha kutakuwa hamna shughuli za sherehe zozote mpaka Corona itakapokuwa haipo tena au itakapokuwa imedhibitiwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tarime Mhandisi Mtemi Msafiri ameeleza kuwa kwa sasa wamebaini baadhi ya wazazi wanawapeleka watoto wao ambao ni wanafunzi kukeketwa na kuwaozesha katika kipindi hiki.

“Ofisi yangu bado inafuatilia suala hili, na nitoe rai kama jambo hili ni la kweli liachwe mara moja ili kuwalinda watoto waweze kuendelea na masomo yao” alisema Eng. Msafiri.

Mkoa wa Mara kwa sasa una watu waliopo karantini baada ya kusafiri nje ya nchi na hauna mgonjwa aliyethibitika kuwa na Corona baada ya mgonjwa aliyekuwepo kupona na kurudi nyumbani kwake katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Serikali imefunga shule na vyuo vyote kwa muda usiojulikana ili kuweza kuepusha mikusanyiko inayoweza kusababisha maambukizi ya virusi vya Corona kwa wanafunzi.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.