Thursday 24th, April 2025
@Mkoa wa Mara
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara katika Mkoa wa Mara kuanzia tarehe 4 -7 Februari, 2022. Katika Ziara hiyo Mheshimiwa Rais atashiriki matembezi na kilele cha miaka 45 ya Chama cha Mapinduzi, kuweka jiwe la msingi katika Mradi wa Maji wa Mgango -Kiabakari, kuweka jiwe la msingi katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, kutembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa, kuweka jiwe la Msingi katika Chujio la Mradi wa Maji Bunda (Nyabehu) na kuzungumza na wananchi katika maeneo ya Kiabakari (Butiama), Uwanja wa Karume, Mgango (Musoma Vijijini) na Bunda Mjini. Wote mnakaribishwa
Katibu Tawala Mkoa wa Mara
Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara
Telephone: +255282622305
Mobile:
Email: ras.mara@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.