• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Tumieni magari haya kutatua kero za wananchi- Mtambi

Posted on: May 22nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo tarehe 22 Mei, 2025 amekabidhi magari mapya yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan yenye thamani ya shilingi milioni 504 kwa ajili ya Wakuu wa Wilaya za Tarime na Musoma.

Akizungumza wakati wa kukabidhi magari hayo kwa Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka na Mkuu wa Wilaya ya Tarime Meja Edward Gowelle, Mhe. Mtambi amewataka Wakuu wa Wilaya kutumia magari hayo kutatua kero za wananchi katika maeneo yao.

“Tumieni magari haya kuwatembelea wananchi kwa lengo la kusikiliza na kutatua kero za wananchi, kwa sasa hamna kisingizio cha kushindwa kufika sehemu yoyote kwa kuwa haya magari yanapita mahari popote hata ambapo hamna barabara nzuri haya yanapita” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema baada ya Mhe. Rais kutoa magari hayo amemaliza changamoto ya usafiri kwa Wakuu wa Wilaya ambapo awali magari kwa baadhi ya Wakuu wa Wilaya yalikuwa yanazimwa kutoka katika taasisi nyingine za umma lakini kwa sasa Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa Mara wanayo magari mapya waliyonunuliwa na Mhe. Rais.

Mhe. Mtambi amewataka Wakuu wa Wilaya kuyatunza magari hayo na kuhakikisha wanasimamia madereva wanayoyaendesha magari hayo ili waweze kuchukua tahadhari katika uendeshaji wao na kufuatilia ratiba za matengenezo ya kawaida ya magari hayo.

Kanali Mtambi ametumia fursa hiyo na kuwataka Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Mara kutumia magari hayo kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 ili waweze kuchagua viongozi bora wanaopenda maendeleo.  

Akizungumza katika hafla ya mapokezi ya gari hizo, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Meja Edward Gowelle ameishukuru Serikali kwa kupatiwa magari ambayo yatawawezesha kufika katika maeneo yao ya utawala kwa haraka na kuwahudumia wananchi.

“Haya magari yatatusaidia sana kuwafikia wananchi na kusikiliza na kutatua kero zao, kukagua miradi ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa katika Wilaya zetu na yataongeza kasi yetu katika kuwahudumia wananchi” amesema Mhe. Gowelle.

Mhe. Gowelle ameahidi kuwa watayatumia magari hayo kama yalivyokusudiwa na watasimamia kuhakikisha yanatunzwa na kutumika kwa shughuli za Serikali katika kuwahudumia wananchi na kuahidi kuyatunza ili yaweze kudumu muda mrefu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka watatekeleza maagizo yote ya Mkuu wa Mkoa na kuhakikisha magari hayo yanaleta tija kwa wananchi.

“Tunashukuru sana kwa kupatiwa magari haya ambayo yatatusaidia kufuatilia utekelezaji wa miradi na kutatua kusikiliza kero za wananchi kwa wakati” amesema Mhe. Chikoka.  

Hafla ya kukabidhi magari hayo imehudhuliwa na Wakuu wa Wilaya, watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala wa Wilaya na baadhi ya watumishi kutoka Ofisi za Wakuu wa Wilaya waliopokea magari hayo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Tumieni magari haya kutatua kero za wananchi- Mtambi

    May 22, 2025
  • CCM yapongeza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Mara

    May 20, 2025
  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa