• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awapongeza 2,891 kwa kupata daraja la kwanza

Posted on: July 8th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 8 Julai, 2025 amepokea taarifa mbalimbali za Sehemu ya Elimu na kuwapongeza wanafunzi 2,891 wa Mkoa wa Mara waliopata ufaulu wa daraja la kwanza katika matokeo ya mtihani wa Kitaifa wa kidato cha sita yaliyotangazwa tarehe 7 Julai, 2025.

Mhe. Mtambi ametoa pongezi hizo baada ya kuarifiwa kuwa jumla ya wanafunzi 2,891 ambao ni sawa na asilimia 61.4 ya wanafunzi wote 4,708 wa Mkoa wa Mara waliofanya mtihani wa kidato cha sita wamefaulu na kupata daraja la kwanza.

“Ninapongeza sana kwa matokeo haya, shule zimejitahidi sana kuwasimamia wanafunzi vizuri na wanafunzi wote wamefaulu vizuri, hongereni sana” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi ameitaka Sehemu ya Elimu kuandaa kikao cha tathmini ambacho kitatumika pia kuzipongeza shule, walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani huo hata hivyo amesema zawadi ya gari haitatolewa kwa kuwa hamna shule iliyoingia katika 10 bora za kitaifa.  

“Kwa sasa Mkoa utatoa zawadi za kawaida hadi hapo shule zitakapofanya vizuri zaidi Mkoa utatoa zawadi ya gari kwa shule zitakazoingia kwenye 10 bora za kitaifa na hili linawezekana” amesema Mhe. Mtambi.

Aidha, Mhe. amewapongeza walimu na wanafunzi waliohusika na mtihani huo kwa kupata matokeo mazuri ambapo wanafaunzi waliopata daraja la pili ni 1,597 ambayo ni sawa na asilimia 33.9 na waliopata daraja la tatu ni 220 ambao ni sawa na asilimia 4.67 ya wanafunzi wote waliofanya mtihani huo.   

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Mwalimu Makwasa Bulenga amesema kuwa Mkoa wa Mara ulikuwa na jumla wanafunzi 4,708 waliofanya mtihani huo kutoka Shule za Sekondari 29 na wote wamepata ufaulu wa daraja la kwanza hadi la tatu pekee.

Bwana Bulenga amesema shule iliyoongoza kwa ufaulu ni Shule ya Sekondari ya Bunda (Bunda) ambayo imeshika nafasi ya 25 kitaifa na nafasi ya saba kwa shule za Serikali kitaifa na kufuatiwa na Shule ya Sekondari Mkono (Butiama) na Shule ya Sekondari ya Tarime (Tarime).  

Bwana Bulenga amesema katika Shule za Sekondari za Bunda na Mkono wanafunzi waliopata ufaulu wa daraja la kwanza ni asilimia 91 ya wanafunzi wote waliofanya mtihani huo na kuzipongeza shule hizo kwa kufanya vizuri.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Shule za Sekondari za Mkono (Butiama), Morembe Day (Manispaa ya Musoma), Busegwe, Chiefu Ihunyo na Kiagata (Butiama) na Nyamunga (Rorya) wanafunzi wake wamepata ufaulu wa daraja la kwanza na la pili pekee.

Aidha, Bwana Bulenga amesema asilimia 45 ya watahiniwa waliofanya mtihani huo walichaguliwa kuanza kidato cha tano wakiwa na ufaulu wa daraja la tatu na wengi wao sasa wamepata daraja la kwanza na la pili.

Bwana Bulenga amesema Mkoa umepata ufaulu wa asilimia 100 huku Mkoa wa Mara ukiwa na wastani wa GPA 2.059 na kati ya shule 29 zilizoshiriki mtihani huo, shule 23 zikiwa ni za Serikali na shule sita za binafsi.   

Tukio hilo lilihudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Ndugu Gerald Musabila Kusaya, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu, baadhi ya maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na wajumbe wa Kamati ya Wataalamu waliokagua miradi ya mbio za Mwenge katika Mkoa wa Mara.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi ataka maboresho maandalizi ya UMISETA/UMETASHUMTA

    July 08, 2025
  • Mtambi awapongeza 2,891 kwa kupata daraja la kwanza

    July 08, 2025
  • Mita mpya kupunguza malalamiko ya bili za maji- BUWSSA

    July 04, 2025
  • Chanjo na Utambuzi wa mifugo kuwanufaisha wafugaji -Dkt. Ashatu

    July 04, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa