• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi ataka maboresho maandalizi ya UMISETA/UMETASHUMTA

Posted on: July 8th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara leo amepokea makombe ya ushindi ya mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) na Umoja wa Michezo Shule za Sekondari Tanzania (UMISETA) kitaifa na kutaka Mkoa kuboresha maandalizi ya ushiriki katika mashindano hayo ili kufanya vizuri zaidi.

Akizungumza mara baada ya kupokea vikombe hivyo, Mhe. Mtambi amezipongeza timu za Mkoa kwa kufanya vizuri katika mashindano hayo na kuutaka Mkoa kuboresha zaidi maandalizi ya wananfunzi wanaoshiriki michezo ili kupata timu bora zaidi.

“Katika historia ya michezo hapa nchini, Mkoa wa Mara umekuwa ukitoa wachezaji wazuri sana, tujipange vizuri na tuboreshe maandalizi yetu tunaweza kufanya vizuri zaidi” amesema Mhe. Mtambi.

Aidha, Mhe. Mtambi ameitaka Sehemu ya Elimu kuwaendeleza wanafunzi wenye vipaji katika michezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwaunganisha na vyama vya michezo hiyo ili kuendeleza vipaji vya wanafunzi hao.

Akitoa taarifa ya mashindano hayo, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Mwalimu Makwasa Bulenga amesema Mkoa wa Mara umefanikiwa kupata jumla ya makombe sita na medali 50 ambapo makombe matano na medali 31 yametokana na UMITASHUMTA na kombe moja na medali 19 limetokana na UMISETA.  

Bwana Bulenga amesema katika mashindano ya UMITASHUMTA Mkoa umeshika nafasi ya 2 Kitaifa kati ya mikoa 31 iliyoshiriki katika mashindano ya UMITASHUMTA na nafasi ya 17 kitaifa kati ya mikoa 28 iliyoshiriki katika mashindano ya UMISETA.

“Michezo tuliyofanya vizuri ni riadha wanawake, riadha wanaume, soka wanawake, handball wanawake na usafi na nidhamu wanaume katika UMITASHUMTA na katika UMISETA Mara iliongoza katika riadha wanaume” amesema Mwalimu Bulenga.  

Bwana Bulenga amesema ili kupata matokeo mazuri miaka inayokuja, Mkoa utaweka mkazo katika kuimarisha vitalu vya michezo ili kuwaandaa wachezaji wenye vipaji, kuongeza usimamizi wa wanamichezo katika Shule za Sekondari, kuongeza miundombinu na vifaa vya michezo katika shule zote za Mkoa wa Mara.

Mashindano ya 29 ya UMITASHUMTA na mashindano ya 45 UMISETA yalifanyika katika Manispaa ya Iringa na kufunguliwa rasmi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa tarehe 09 Juni, 2025 na kufungwa rasmi na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Said Omar Kipanga tarehe 18 Juni, 2025.

Mashindano ya 45 ya UMISETA yalifungwa rasmi tarehe 29 Juni, 2025 na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Festo Dugange yakiwa na kauli mbiu isemayo “viongozi bora ni msingi wa Maendeleo ya Taaluma, Sanaa na Michezo, Shiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa Amani na Utulivu”.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amepokea taarifa ya Kamati ya Wataalamu iliyoundwa kufuatilia miradi ya Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Mara na kuipongeza kamati hiyo kwa kazi nzuri waliyoifanya na kuahidi kuyafanyia kazi baadhi ya mapungufu yaliyobainika katika maandalizi ya mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2025.  

Aidha, amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa Ndugu Gerald Musabila Kusaya kufuatilia miradi iliyopangwa kutembelewa na Mwenge ambayo ilibainika kuwa na changamoto mbalimbali katika Halmashauri za Mkoa wa Mara ili iweze kufanyiwa kazi na kufuatiliwa ukamilishaji wake.

Mkoa wa Mara unatarajiwa kupokea Mwenge wa Uhuru tarehe 15 Agosti, 2025 kutoka Mkoa wa Simiyu ambapo utakimbizwa katika Halmashauri zote tisa kabla ya kukabidhiwa Mkoa wa Mwanza kuendelea na mbio zake.

Tukio hilo lilihudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Ndugu Gerald Musabila Kusaya, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu, baadhi ya maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na wajumbe wa Kamati ya Wataalamu waliokagua miradi ya mbio za Mwenge katika Mkoa wa Mara.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi ataka maboresho maandalizi ya UMISETA/UMETASHUMTA

    July 08, 2025
  • Mtambi awapongeza 2,891 kwa kupata daraja la kwanza

    July 08, 2025
  • Mita mpya kupunguza malalamiko ya bili za maji- BUWSSA

    July 04, 2025
  • Chanjo na Utambuzi wa mifugo kuwanufaisha wafugaji -Dkt. Ashatu

    July 04, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa