• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yaweka Mikakati ya UVIKO 19

Posted on: July 19th, 2021

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela amewataka wasimamizi wa huduma za Afya katika Mkoa wa Mara kutengeneza na kuja na  mkakati madhubuti wa namna bora ya kuendelea kupambana na maambikizi ya  uviko 19 katika Mkoa wa Mara.

Bwana Msovela ametoa kauli hiyo leo tarehe 16 Julai 2021 wakati wa kikao cha Timu ya Usimamizi wa Huduma za afya ngazi ya Mkoa na Halmashauri kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Waganga Musoma (COTC) ili kujadili na kuweka mikakati ya kukabiliana na Uviko 19.

"Tunapotoka hapa kama wataalamu tunaohusika na masuala ya Afya ndani ya Mkoa inabidi tutengeneze mapendekezo na maazimio juu ya namna ya kupambana na Uviko 19 ili itusaidie katika kuona namna gani Mkoa unaweza kupunguza maambukiziā€ alisema Bwana Msovela  na kuwataka waendelee kutoa huduma huku wakizingatia njia za kujikinga na maambukizi kwa sababu Watumishi wakichukua tahadhari hata wananchi wengine wataiga kutoka kwao maana mabadiliko yoyote yanaanza na watendaji kabla ya kufika kwa wananchi.

"Wataalamu tunapotoa huduma tuzingatie njia za kutumia katika kujiepusha  na janga la Corona kwa kuvaa barakoa, kunawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka na sabuni, kukaa umbali unaohitajika na kuepuka misongamano isiyo ya lazima.

Aidha amewataka  wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kuhusu kujikinga na janga la Corona kwa kuendelea kufuata ushauri na elimu inayotolewa na wataalamu wa Afya ikiwemo kuepuka misongamano isiyo ya lazima, kunawa mikono kwa kutumia maji tiririka, kutumia vitakasa mikono na kuvaa barakoa.

Katika hatua nyingine Katibu Tawala amewataka Watumishi wa sekta ya Afya kufanya kazi kwa upendo, ushirikiano na kuthaminiana kila mmoja katika nafasi yake ili katika utekelezaji wa majukumu kuwepo na mnyororo wa uelewa kuanzia ngazi ya juu hadi chini.

Aidha, amewataka Waganga Wakuu wa Halmashauri kuhakikisha katika kila kituo Cha kutolea huduma za Afya kunafungwa mfumo wa kielektroniki wa ukusanyaji wa mapato (GOTHOMIS) ili kuepusha mianya ya wizi na upotevu wa mapato ya serikali.

Awali akimkaribisha Katibu Tawala, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Frolian Tinuga amesema kuwa wagonjwa wa Corona katika Mkoa wa Mara wapo na jitihada za kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya namna ya kukabiliana na maambukizi zinafanyika hivyo kikao hiki kina lengo la kuweka mapendekezo na maazimio ya namna bora ya kuboresha zaidi mfumo na njia za kupambana na maambukizi kwa wananchi.

"Hakuna njia mpya za kujikinga na Uviko 19 zaidi ya zile zilizopo lakini kukutana kwetu inabidi tuweke maazimio na mikakati itakayoboresha na kutuwezesha kukabiliana na maambukizi kwa kuwafikia wananchi wote na kuwapatia elimu ya namna ya kupambana na ugonjwa huu.

Sambamba na hilo Dkt. Frolian amewaagiza wasimamizi wa huduma za Afya ngazi ya Halmashauri kuendelea kutoa Elimu kwa wananchi kuhusu kujikinga na Uviko 19 kwa kutembelea maeneo yenye mikusanyiko kutumia radio, magari ya matangazo pamoja na kuhakikisha  katika vituo vyote vya kutokea huduma za Afya kunakuwepo njia zote za kujikinga na maambukizi ikiwemo uwepo wa  maji ya kunawa na sabuni,vitakasa mikono pamoja na kusisitiza wahudumu wote na wananchi kuvaa barakoa pindi watoapo na kupata huduma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi ataka maboresho maandalizi ya UMISETA/UMETASHUMTA

    July 08, 2025
  • Mtambi awapongeza 2,891 kwa kupata daraja la kwanza

    July 08, 2025
  • Mita mpya kupunguza malalamiko ya bili za maji- BUWSSA

    July 04, 2025
  • Chanjo na Utambuzi wa mifugo kuwanufaisha wafugaji -Dkt. Ashatu

    July 04, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa