• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

Posted on: May 15th, 2025

Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Utafiti na Masoko wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bwana Mrisho Mrisho amesema Mkoa wa Mara una fursa nyingi kwa kazi za Sanaa kutokana na kuwepo kwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na migodi mikubwa ya madini.

“Mkoa wa Mara kupitia fedha za uwajibikaji kwa jamii, tozo na makusanyo mengine unatakiwa kuona namna ya kutumia fedha hizo kuibua na kukuza vipaji vya sanaa kwa vijana wadogo tangu ngazi ya shule” amesema Bwana Mrisho.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha mafunzo ya siku mbili kwa Maafisa Biashara kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Mara Bwana Mrisho amesema faida kubwa ya mifumo ya Serikali kusomana kuwa ni pamoja na kuongeza ufanisi wa kazi na kuondoa usumbufu kwa wasanii na wadau wengine.

Bwana Mrisho amesema awali mifumo ilikuwa haisomani na kusababisha wadau ikiwemo wasanii kudanganywa na kupewa vibali feki jambo ambalo amesema kwa sasa halipo tena baada ya Serikali kurekebisha tatizo hilo.

Ndugu Mrisho amesema taasisi ikishasajiliwa na BASATA inapata faida nyingi kwa kuwa BASATA ina aina zote za wataalamu kutoka idara kadhaa ikiwamo ya sheria, mipango na TEHAMA wanaomsaidia mteja kwa kumpa ushauri wa bure wa kitaalamu na kumwezesha kufanyakazi kwa uhuru.

Kwa upande wake Afisa Utamaduni Mkoa wa Mara mwalimu Makondo Makondo ameishukuru BASATA kwa kuwawezesha wataalamu wa Mkoa wa Mara kupata mafunzo hayo ili kuweza kuwasaidia wasanii mbalimbali waliopo katika Mkoa.

Bwana Makondo amesema kuwa kwa maazimio haya waliyokubaliana katika mafunzo haya sasa Mkoa wa Mara unaweza kuwa na matamasha makubwa ya Kitaifa katika ngazi za Shule za Msingi na Sekondari.

Bwana Makondo amesema shule zina vilabu vya masuala mbalimbali ikiwemo kupinga rushwa, mazingira na michezo ambavyo vinafanya vizuri sana mashuleni na kupendekeza kuanzishwa klabu mahususi ya masuala ya Sanaa ili wanafunzi waweze kujifunza wakiwa wadogo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • RC Ampokea Meja Jenerali Mani

    May 13, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa