Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mstaafu, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Mei 25, 2025 ameongoza harambee katika Kanisa la Mtakatifu Petro, Parishi ya Bunda, Dayosisi ya Mara ya Kanisa la Angikana la Tanzania na kufanikisha kukusanya shilingi milioni 205.
Akizungumza katika harambee hii iliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Bunda, Mhe. Dkt. Kikwete amewaomba Watanzania kuendelea kuwa na mshikamano wa Kitaifa kama ilivyo desturi ya kutobaguana, ndiyo maana na yeye japokuwa ni Muisilamu lakini amekuja kuongoza Harambee ya ujenzi wa Kanisa la Mtakatifu Petro ili kanisa hilo linafanane na heshima ya Mtakatifu Petro ilivyo.
“Kweli Kanisa lenu lile ni dogo hata Mtakatifu Petro huko alipo atakuwa anasikitika, lazima lijengwe kanisa la kubwa lenye hadhi yake na ndiyo maana na mimi nipo hapa” amesema Mhe. Kikwete.
Mhe. Dkt. Kikwete amesema watu wa Mkoa wa Mara ni wakalimu na wanapenda watu hata mdogo wake aliwahi kuoa Mkoani Mara, huku akisimulia kuwa yeye binafsi anaujamaa wa karibu na watu wa Mkoa huu.
Akizungumza wakati wa kumkaribisha Dkt. Kikwete, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi amesema hali ya Mkoa wa Mara ni salama na tulivu, huku wakiendelea kusimamia miradi kadhaa ya maendeleo kutoka Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan.
Mhe. Mtambi amemkaribisha na kumshukuru Mhe. Kikwete kwa kutembelea na kuongoza harambee hiyo katika Mkoa wa Mara.
Mhe. Mtambi ametumia pia fursa hiyo kuwakumbusha waumuni wa Kanisa la Anglikana kuwahamasisha wananchi kuhusu kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa amani na utulivu.
Kwa upande wao viongozi wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Mara na Dayosisi kando kando walioshiriki Harambee hii wamemshukuru Dkt. Kikwete kwa kuongoza na kufanikisha kupatikana pesa hizo.
Katika harambee hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amechangia shilingi milioni 50 wakati Mkuu wa Mkoa wa Mara akichangia shilingi milioni 15 katika harambee hiyo.
Katibu Tawala Mkoa wa Mara
Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara
Simu: +255282622305
Simu:
Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz
Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa