• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kikwete achangisha milioni 200 za ujenzi wa kanisa Mara

Posted on: May 26th, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mstaafu, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Mei 25, 2025 ameongoza harambee katika Kanisa la Mtakatifu Petro, Parishi ya Bunda, Dayosisi ya Mara ya Kanisa la Angikana la Tanzania na kufanikisha kukusanya shilingi milioni 205.

Akizungumza katika harambee hii iliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Bunda, Mhe. Dkt. Kikwete amewaomba Watanzania kuendelea kuwa na mshikamano wa Kitaifa kama ilivyo desturi ya kutobaguana, ndiyo maana na yeye japokuwa ni Muisilamu lakini amekuja kuongoza Harambee ya ujenzi wa Kanisa la Mtakatifu Petro ili kanisa hilo linafanane na heshima ya Mtakatifu Petro ilivyo.

“Kweli Kanisa lenu lile ni dogo hata Mtakatifu Petro huko alipo atakuwa anasikitika, lazima lijengwe kanisa la kubwa lenye hadhi yake na ndiyo maana na mimi nipo hapa” amesema Mhe. Kikwete.

Mhe. Dkt. Kikwete amesema watu wa Mkoa wa Mara ni wakalimu na wanapenda watu hata mdogo wake aliwahi kuoa Mkoani Mara, huku akisimulia kuwa yeye binafsi anaujamaa wa karibu na watu wa Mkoa huu.

Akizungumza wakati wa kumkaribisha Dkt. Kikwete, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi amesema hali ya Mkoa wa Mara ni salama na tulivu, huku wakiendelea kusimamia miradi kadhaa ya maendeleo kutoka Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Mtambi amemkaribisha na kumshukuru Mhe. Kikwete kwa kutembelea na kuongoza harambee hiyo katika Mkoa wa Mara.

Mhe. Mtambi ametumia pia fursa hiyo kuwakumbusha waumuni wa Kanisa la Anglikana kuwahamasisha wananchi kuhusu kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa amani na utulivu.

Kwa upande wao viongozi wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Mara na Dayosisi kando kando walioshiriki Harambee hii wamemshukuru Dkt. Kikwete kwa kuongoza na kufanikisha kupatikana pesa hizo.

Katika harambee hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amechangia shilingi milioni 50 wakati Mkuu wa Mkoa wa Mara akichangia shilingi milioni 15 katika harambee hiyo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • Waongozeni wanafunzi kufikia ndoto zao- Kusaya

    May 29, 2025
  • Kamati za Maafa Mkoa wa Mara zajengewa Uwezo

    May 26, 2025
  • Kikwete achangisha milioni 200 za ujenzi wa kanisa Mara

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa