• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TANAPA kuboresha Shule ya Msingi ya Kenyamusabi

Posted on: March 5th, 2021

Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) imeahidi kuiboresha Shule ya Msingi Kenyamusabi iliyopo katika Wilaya ya Tarime Mkoa wa Mara ikiwa ni sehemu ya maridhiano kati ya wananchi na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA).

Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Kanda ya Magharibi wa TANAPA Bwana Martin Loibooki ameeleza kuwa kwa kuanzia TANAPA itatoa shilingi milioni 10 kwa ajili ya kumalizia vyumba viwili vya madarasa vilivyoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi katika shule hiyo.

“Mpango wetu ni kutenga fedha zaidi kwa ajili ya kujenga vyumba zaidi vya madarasa na kuyakarabati majengo ya shule yaliyopo katika bajeti ya TANAPA ya mwaka 2021/2022 ambayo inaendelea kuandaliwa” alisema Bwana Loibooki.

Aidha ameeleza kuwa TANAPA inampango wa kuendelea kuimarisha mahusiano na wananchi wa eneo hilo ambalo limekuwa na migogoro ya mara kwa mara kati ya wananchi na SENAPA kutokana na masuala ya kugombea mipaka, uwindaji haramu ndani ya hifadhi, wananchi kuharibu miradi iliyotengenezwa na SENAPA nakadhalika.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ambaye aliongoza kikao hicho cha maridhiano leo tarehe 3 Machi 2021 ameeleza kuwa wananchi wakishiriki ipasavyo kwenye ulinzi wa hifadhi ya Serengeti watafaidika na mambo mengi sana ikiwemo uboreshaji wa huduma za kijamii katika eneo hilo.

“Nimefurahishwa sana na TANAPA kukubali ombi la wananchi la kuiboresha shule hii ili wananchi na watoto wanaosoma hapa waone kuwa wanafaidika na kuwepo kwa hifadhi karibu na maeneo yao na sio hadithi tu”alisema Mheshimiwa Malima.   

Aidha Mheshimiwa Malima amewahakikishia wananchi kuwa uchunguzi wa tukio la kupotea kwa Bwana Manga Kahuru Manga unaendelea na timu ya wataalamu wanaendelea kuchunguza na matokeo ya uchunguzi yatawasilishwa kwao mara baada ya uchunguzi kukamilika.

“Ninawaomba muendelee kutoa ushirikiano kwa timu ya uchunguzi  wa tukio hilo ili tuweze kupata ufumbuzi wa tukio la kupotea kwa kijana huyu kwa haraka” alisema Mheshimiwa Malima.

Kijana Manga Kahuru Manga mwenye umri wa miaka 20 alipotea wakati akiwa anachunga ng’ombe na mwezie ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti tarehe 11 Desemba 2020 na mpaka sasa uchunguzi bado unaendelea.

Katika kikao hicho wananchi pamoja na diwani wa eneo hilo Mheshimiwa Ayoub Marwa walifurahishwa na ahadi hiyo ya TANAPA na kuahidi kutoa ushirikiano kwa TANAPA katika kuimarisha mahusiano yaliyopo kati ya hifadhi na wananchi wa eneo hilo.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa