• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara wapatiwa mafunzo

Posted on: June 20th, 2025

Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara leo tarehe 20 Juni, 2025 wamejengewa uwezo kuhusu Mkakati wa Taifa wa Kupambana na Rushwa, masuala mbalimbali ya kiutumishi, huduma zinazotolewa na Shirika la Bima ya Maisha la SANLAM na Benki ya NMB katika mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa uwekezaji.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Dkt. Zabron Masatu amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo watumishi kuhusiana na masuala ya rushwa na namna ya kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Kupambana na Rushwa katika maeneo ya kazi.

“Lengo la mafunzo haya ni kukumbushana masuala muhimu katika utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Kupambana na rushwa katika taasisi yetu na hususan mwaka huu tunapoelekea katika uchaguzi mkuu” amesema Dkt. Masatu. 

Dkt. Masatu ameishukuru Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara pamoja na wadau wengine waliofika kwa ajili ya kutoa mafunzo hayo muhimu kwa watumishi na kuwataka watumishi kufuatilia kwa ukaribu na kuyazingatia mafunzo hayo katika utendaji wao wa kazi.  

Aidha, Dkt. Masatu ameishukuru Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu kwa kuandaa mafunzo hayo muhimu kwa ajili ya watumishi na kuitaka Idara hiyo kuandaa tena wakati mwingine mafunzo kuhusu magari kwa ajili ya madereva.

Akiwasilisha mada katika mafunzo hayo, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mara Bwana Mohamed Shariff amesema wadau mbalimbali wanawajibu wa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Kupambana na Rushwa katika taasisi zao na hivyo kuitaka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kutekeleza majukumu yake kulingana na mwongozo wa mkakati huo.

Bwana Shariff amesema chanzo kikuu cha rushwa ni ukiukwaji wa maadili kwa maslahi binafsi na ili kupunguza tatizo la rushwa sehemu za kazi, Serikali ilitoa mwongozo wa kila taasisi kuwa na Kamati Maalum ya Menejimenti na Kamati ya Uadilifu ili malalamiko ya ndani na nje ya taasisi yaweze kufanyiwa kazi na mianya ya rushwa kuzibwa.

Watumishi pia wamejengewa uwezo kuhusu ujazaji wa taarifa katika mfumo wa PEPMIS, utunzaji wa magari, mabadiliko ya muundo wa Ofisi za Wakuu wa Mikoa yatakayoanza Julai, 2025, uandaaji wa taarifa baada ya kufanya ufuatiliaji katika Wilaya na Halmashauri. 

Aidha, watumishi hao wamepewa pia mafunzo kuhusu huduma zinazotolewa na Shirika la Bima ya Maisha la SANLAM na Benki ya NMB na kuhamasishwa kuchangamkia fursa mbalimbali zitolewazo na taasisi hizo.

Mafunzo hayo yamehudhuriwa na Wakuu wa Idara na Vitengo, Makatibu Tawala wa Wilaya, watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na ofisi za Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Mara, maafisa kutoka TAKUKURU, Benki ya NMB na Shirika la Bima la SANLAM. 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara wapatiwa mafunzo

    June 20, 2025
  • Mara mshindi wa pili UMITASHUMTA 2025

    June 18, 2025
  • Zingatieni miongozo ya kilimo cha tumbaku- Dkt. Haule

    June 18, 2025
  • Mtambi aipongeza Bunda TC kwa hati safi miaka mitano mfululizo

    June 13, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa