• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Vijana changamkieni fursa

Posted on: July 27th, 2024

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru godfrey eliakimu mzava amewataka vijana kuachana na mambo yasiyo na tija wajiunge kwenye vikundi vy uzalishaji mali na kuchangamkia fursa za mikopo inayotolewa na Serikali kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Ndugu Mzava ametoa rai hiyo wakati akizungumza na vijana baada ya kukagua mradi wa kikundi cha vijana cha Eden Group katika Kijiji cha Muriba, Kata ya Muriba Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wakati Mwenge wa Uhuru ukiendelea na mbio zake katika Wilaya ya Tarime.

“Kikundi hiki kinaundwa na viwanja watano wenye elimu ya Chuo Kikuu na mmoja chuo cha kati ambao walijiunga na kukopeshwa shilingi milioni sita na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime mwaka 2023 ambao mpaka sasa wamesharejesha fedha zote za Halmashauri na biashara yao inaendelea vizuri” amesema Bwana Mzava.

Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa amewapongeza vijana hao kwa kuungana pamoja katika mambo ya kujiletea maendeleo na kuanzisha biashara ambayo inaendelea vizuri na kumtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime mikopo itakapofunguliwa tena, kikundi hicho kipewe kipaumbele.

Bwana Mzava amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kutoa kipaumbele cha mikopo kwa vikundi vinavyowahi kurejesha mikopo ya makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu ili waweze kuendelea kufanya shughuli za uzalishaji mali na kupunguza tatizo la ajira katika jamii.  

Kwa upande wake, Katibu wa Kikundi cha Eden Group Bwana Amos Lameck Gisiri amesema kikundi hicho kilianzishwa mwaka 2022 na kusajiliwa na Halmashauri hiyo kikiwa na wanachama watano na kati yao wanne wakiume na mmoja wakike.

Bwana Gisiri amesema kikundi chao kinajishughulisha na biashara ya vifaa vya umeme wa majumbani na viwandani na kiliwahi kukopeshwa na Halmashauri mwaka 2023 ambapo walirejesha mkopo na kwa sasa biashara yao ina mtaji wa shilingi 7,200,000.

“Lengo la kikundi ni kuwa na kampuni kubwa ya uuzaji na usambazaji wa vifaa vya umeme Wilayani Tarime” amesema Bwana Gisiri na kuongeza kuwa kwa sasa pamoja na duka hilo wameshafungua duka jingine katika kijiji cha Gibaso na kutoa ufadhili wa elimu kwa kijana mmoja kusomea Chuo cha Lubondo Biharamulo.

Mwenge wa Uhuru unaendelea na Mbio zake katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime baada ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime Bibi Angelina Lubella Marko kukabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime Bwana Saul Mwaisenye katika Kijiji cha Kerende, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Miradi mingine ambayo imetembelewa na kukaguliwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ni pamoja na jengo la biashara la Nyamongo Plaza ambao umezinduliwa, mradi wa maji Nyangoto ambao umetembelewa kuangaliwa uendelevu wake baada ya kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2023, mradi wa Bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Nyamwaga.

Miradi mingine itakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru leo ni nyumba ya mtumishi ya 2 in one katika Kituo cha Afya Magoto, ujenzi wa daraja la Kebweye na mradi wa uhifadhi wa mazingira katika Shule ya Sekondari ya Nyasaricho.

 Mkesha wa Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kuwa katika Uwanja wa Tarafa katika eneo la Sirari na kesho Mwenge unatarajiwa kukabidhiwa katika Halmashauri ya Mji wa Tarime.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa