• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Uwanja wa Ndege kuifungua Mara kiuchumi

Posted on: August 6th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameelezea matumaini yake kuwa Uwanja wa Ndege wa Musoma utakapokamilika utaufungua Mkoa wa Mara kiuchumi.

Mheshimiwa Hapi ametoa matumaini hayo leo tarehe 3 Agosti 2021 wakati wa ziara yake aliyoifanya katika Manispaa ya Musoma kukagua miradi ya maendeleo.

“Huu uwanja ukikamilika ndege kubwa za abiria na mizigo zitatua hapa na hivyo kuwaleta watalii kutua Musoma halafu kuingia katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kusafirisha samaki kutoka viwandani moja kwa moja bila kuhitajika kupitia Mwanza” alisema Mheshimiwa Hapi.

Ameeleza kuwa kutokana na utajiri mkubwa uliopo Mkoa wa Mara na miradi mikubwa inayojengwa ikiwemo Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere cha Kilimo, Sayansi na Teknolojia uwanja wa ndege utafungua zaidi mirango ya kiuchumi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kutokana na historia ya uwanja huo kwa taifa la Tanzania, kukarabatiwa kwake ni sehemu ya kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye alikuwa akiutumia uwanja huo mara kwa mara akiwa hai.

“Hata wakati wa vita vya Kagera, uwanja huu ulitumika katika kusafirisha wapiganaji na mizigo kwenda Uganda kwa wakati huo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Ameahidi kufuatilia malipo ya awali ya mkandarasi katika Wizara ya Ujenzi na Usafirishaji ili kazi ya ukarabati wa uwanja huo iweze kuanza mara moja.

Hatua iliyofikia kwa sasa Mkandarasi ameleta vifaa vya ujenzi na anaendelea na ujenzi wa ofisi za muda atakazozitumia wakati wa utekelezaji wa mradi huo.

Akitoa taarifa ya Mradi huo Meneja wa TANROADS Mhandisi Mlima Ngaile  ameeleza kuwa kazi zitakazofanyika ni pamoja na kukarabati njia ya kutua na kurukia ndege kuwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilomita 1.705.

“Kazi nyingine ni ukarabati na uboreshaji wa maungio (tax way),ukarabati wa maegezo ya ndege, uzio wa usalama, ujenzi wa miundombinu ya kuondoa maji yasituame, ujenzi wa jengo la zimamoto, ununuzi wa gari la zimamoto, ujenzi wa kituo cha umeme na ununuzi wa genereta” alisema Mhandisi Ngaile.

Ameeleza kuwa kazi nyingine ni ujenzi wa jengo la muda la waongoza ndege, ununuzi na ufungaji wa mitambo ya radio call.  

Mkataba ulisainiwa tarehe 28 Desemba 2020 na mkandarasi alikabidhiwa eneo la ujenzi tarehe 30 Aprili 2021 na mkandarasi alipewa miezi mitatu ya kujiandaa kwa kazi ya ujenzi ambapo ilikamilika tarehe 30 Julai 2021.

Kwa muUtekelezaji wa mradi huu kwa mujibu wa mkataba ni wa miezi 20 na utakapokamilika utaruhusu ndege kubwa za abiri na mizigo kuanza kutua katika uwanja huo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa