• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Tatueni Changamoto za mradi wa hospitali- Hapi

Posted on: August 16th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kutatua changamoto mbalimbali zilizojitokeza katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 15 Agosti 2021 wakati alipofanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kukagua miradi ya maendeleo.  

“Nakuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri kukutana na mafundi na vibarua waliokuwa wanajenga katika mradi huu siku ya Jumanne tarehe 17 Agosti 2021 ili kupata ufumbuzi wa madai yao ambayo wameyadai kwa muda mrefu sasa” aliagiza Mheshimiwa Hapi.

Aidha Mheshimiwa Hapi amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kufuatilia madai ya fidia ya mkazi wa eneo hilo ambaye familia yake ilihamishwa kupisha ujenzi wa hospitali hiyo.

“Huyu Mama inasemekana anadai shilingi milioni 22, Halmashauri ipate ushahidi wa uhalali wa deni hilo na kulilipa ili huyu mama apate haki yake kwa wakati apishe katika eneo hili” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi pia ametoa mwezi mmoja wodi za wagonjwa ambazo fedha zake zilikuja tangu Machi 2021 ziwe zimekamilika kujengwa katika hospitali hiyo ili ziweze kuanza kutumika.

Aidha amepinga mapendekezo ya watendaji wa Halmashauri kuwa shilingi milioni 500 iliyopangwa kujenga wodi hizo hazitatosha kujenga wodi tatu na badala yake kuongeza zaidi ya shilingi milioni 200 na kuwataka watendaji hao kukamilisha ujenzi bila kuongeza fedha.

Mheshimiwa Hapi pia ameliagiza Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kupeleka umeme kwenye majengo ya hospitali hiyo ifikapo tarehe 17 Agosti 2021 ili eneo hilo liweze kuwa na umeme.

Katika siku ya kwanza ya ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Mheshimiwa Hapi ametembelea miradi miwili ya ujenzi wa barabara katika eneo la Iramba na Nyamswa, mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi za halmashauri katika eneo la Kibara na mradi wa maji katika eneo la Iramba.

Aidha Mheshimiwa Hapi amezungumza na wananchi katika eneo la Iramba na Nyamswa na kuwataka watendaji kutatua changamoto za wananchi katika maeneo yao.

 Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa ameambatana na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara Mheshimiwa Samweli Kiboye, Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mheshimiwa Joshua Nassari na viongozi pamoja na watendaji wengine wa chama na serikali.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Maambukizi ya UKIMWI katika Wilaya ya Bunda yamepungua

    August 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa