• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU MARA YAKAGUA MIRADI 30

Posted on: November 17th, 2023

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa Wa Mara leo imetoa taarifa kwa Waandishi wa Habari Mkoa wa Mara kuhusu shughuli walizozifanya katika kipindi cha Julai hadi Septemba, 2023 ambapo imekagua miradi 30 yenye thamani ya zaidi shilingi bilioni 12.4 katika sekta za afya, elimu, maji, barabara na utawala.

Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Mara Bwana Fidelis Kalungura na kuwasilishwa kwa waandishi wa habari na  Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mara Bwana Antony Gang’olo imeeleza kuwa jumla ya miradi mitatu kati ya miradi yote iliyokaguliwa ilikutwa na dosari.

Miradi yenye dosari ni pamoja  na mradi wa ujenzi wa miundombinu ya kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari Buturi, Wilaya ya Rorya, ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa na matundu matatu ya vyoo katika Shule ya Msingi Kamimange Wilaya ya Butiama na Ujenzi wa Kituo cha Afya Machochwe.

Bwana Gang’olo ameeleza kuwa katika mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Machochwe “mradi huu umejengwa chini ya kiwango, ununuzi wa vifaa vya ujenzi haukuzingatia mahitaji ambapo baadhi ya vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 6.2 vimebakia, ambayo ni hasara kwa serikali”.

Akizungumzia mradi wa Kituo cha Afya Machochwe, Bwana Gang’olo ameeleza kuwa mradi huo una viashiria vya rushwa na uchunguzi na tayari umeanzishwa.

Aidha katika mradi wa Shule ya Msingi Mamimange Wilaya ya Butiama, vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya shilingi 4,660,000 vilivyonunuliwa viliingizwa katika vitabu lakini havikupokelewa, hali ambayo imechelewesha kukamilika kwa mradi.

Bwana Gang’olo ameeleza kuwa katika mradi wa ujenzi wa miundombinu ya Kidato cha tano na sita katika Shule ya Seondari Buturi, Wilaya ya Rorya, tofali 800 za shilingi 1,600,000 hazikuwa na ubora, TAKUKURU ilielekeza tofali hizo zisitumike katika ujenzi huo na ikawa ni hasara kwa mkandarasi.

Aidha taarifa hiyo imeonyesha kuwa TAKUKURU imefanya uelimishaji wa jamii kupitia njia ya uimarishaji wa klabu za wapinga rushwa 62 za shule za msingi, Sekondari na vyuo vya kati; mikutano ya hadhara 48, semina 45 na imeshiriki katika maonesho tisa na jumla ya watu walioelimishwa katika kipindi hicho ni 9247.

Aidha Bwana Gang’olo ameeleza kuwa jumla ya malalamiko 128 yamepokelewa katika kipindi hicho na kati ya malalamiko hayo, 76 yalihusu vitendo vya rushwa, 52 hayakuhusisha vitendo vya rushwa na malalamiko yote yameshughulikiwa.

Aidha, mashtaka mapya 3, jumla ya kesi 20 ziliendeshwa katika mahakama mbalimbali katika Mkoa wa Mara ambapo  kesi 12 zilitolewa maamuzi na upande wa Jamhuri ilishinda kesi sita na kesi sita  washtakiwa waliachiwa huru.  

Taarifa hii ni mwendelezo wa utaratibu wa kawaida wa TAKUKURU kutoa taarifa za utekelezaji wa majukumu yake katika kira baada ya miezi mitatu.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa