• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Simanieni Huduma za Jamii- Hapi

Posted on: August 16th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kuimarisha usimamizi katika utoaji wa huduma za jamii kwa wananchi.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 14 Agosti 2021 wakati akizungumza na wananchi, viongozi na watumishi katika maeneo tofauti tofauti kazita ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo.

“Serikali imeleta fedha nyingi kwa ajili ya miradi mbalimbali ya huduma za jamii ili wananchi waweze kupata huduma hizo katika maeneo yao bila usumbufu wa kusafiri muda mrefu, simamieni huduma hizo zipatikane” alisema Mheshimiwa Hapi.

Amezitaja huduma ambazo wananchi wanahitaji ziimarike kwa haraka ni elimu, afya, maji, barabara, umeme na ulinzi wao na mali zao.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kwa upande wa elimu, serikali na wananchi wameleta fedha za kujenga miundombinu, serikali imewapandisha madaraja walimu, imeajiri walimu wapya wa masomo ya sayansi ili kuimarisha elimu.

“Sasa kazi yetu ni kuhakikisha maboresho haya makubwa ambayo serikali imeyafanya katika sekta ya elimu yaonekane kwenye matokeo ya mitihani ya wanafunzi, na hayo yatawezekana tu endapo wanaohusika wakisimamia ufundishaji na kudhibiti utoro wa wananfunzi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha katika sekta ya afya, serikali imeongeza miundombinu, bajeti ya dawa, vifaa tiba na kuongeza wataalamu wa afya pamoja na kuwapandisha madaraja watumishi waliokuwa wanastahili.

“Sasa halmashauri ni jukumu lenu kusimamia uboreshaji wa huduma za afya kwa wananchi, udhibiti wa wizi wa dawa na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi katika sehemu zao ili waweze kufanyakazi vizuri” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mheshimiwa Juma Chikoka kusimamia utendaji wa taasisi zilizo katika wilaya yake ambazo zinamajukumu ya kutoa huduma maji, umeme, barabara na kadhalika kwa wananchi.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Rorya Bwana Valentine Deogratius Maganga ameeleza kuwa zama zimebadilika, kwa sasa wananchi wanahitaji maendeleo.

“Sasa sio wakati wa watumishi kukaa maofisini na kuongea tu muda wote, wananchi hawa wanaidai serikali maendeleo ambayo yanapatikana baada ya wataalamu kuyasimamia kwa weredi” alisema Bwana Maganga.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • Waongozeni wanafunzi kufikia ndoto zao- Kusaya

    May 29, 2025
  • Kamati za Maafa Mkoa wa Mara zajengewa Uwezo

    May 26, 2025
  • Kikwete achangisha milioni 200 za ujenzi wa kanisa Mara

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa