• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Simamieni maelekezo ya serikali kuhusu UVIKO 19- Hapi

Posted on: July 27th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amewataka viongozi wa wilaya na wataalamu wa afya kusimamia utekelezaji wa mwongozo uliotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na watoto kuhusu udhibiti wa UVIKO-19.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 27 Julai 2021 wakati akifungua kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi (PHC) kilichofanyika katika ukumbi wa uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Mwongozo ule unamambo mengi mazuri na ya msingi yakisimamiwa tutaweza kupunguza sana kuenea kwa maambukizi ya UVIKO -19 katika mkoa wetu” alisema Mheshimiwa Hapi.

Amesema kwa mfano mwongozo unataka harusi ziahirishwe au kama zitafungwa ziwe na watu wachache, zifanyike maeneo ya wazi na shughuli yote ifanyike ndani ya muda mfupi.

Mheshimiwa Hapi amesema sehemu za biashara zote ziwe na tahadhari za UVIKO 19 ikiwemo maji tiririka ya kunawa, vitakasa mikono, kuzingatia ukaaji kwa nafasi na uvaaji wa barakoa.

“Mkoa wa Mara tupo mpakani tunatakiwa kuongeza juhudi katika udhibiti kwa sababu tupo mpakani na maeneo yetu” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha amewataka wataalamu wa afya kutoa elimu kuhusu chanjo ili itakapofika wananchi watakaoridhia waweze kuipata katika vituo vitakavyobainishwa.

Mkuu wa Mkoa amewataka wataalamu wa afya kutekeleza maelekezo ya serikali kuhusiana na idadi ya watu wanaoenda hospitali kuangalia wagonjwa, utoaji wa matibabu na hususan dozi kwa watu wenye magonjwa ya muda mrefu.

Kwa upande wake Mratibu wa Chanjo Mkoa wa Mara Bi. FLowina Muuzaje ameeleza kuwa chanjo zinatarajiwa kuzinduliwa tarehe 28 Julai 2021 na zinatarajiwa kutolewa bure kwa wananchi watakaoridhia kuchanjwa.

Bi. Muuzaje ameeleza kuwa japokuwa ukichanjwa unaweza kupata tena maambukizi ya UVIKO-19 lakini nguvu ya ugonjwa huo inakuwa imepungua baada ya kupata chanjo kuliko kabla ya chanjo hiyo.

“Chanjo hizi ni salama na zimepitishwa na wataalamu wa afya duniani na zinauwezo wa kupunguza athari za UVIKO- 19 kwa watu wengi zaidi kuliko kabla ya kupata chanjo” alisema Bi. Muuzaje.

 Kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi (PHC) ya Mkoa wa Mara pamoja na mambo mengine kimejadili masuala ya lishe na jitihada za udhibiti wa UVIKO- 19 katika Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa