• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali inampango wa kuibadilisha Musoma

Posted on: October 2nd, 2024

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Boniface Simbachawene leo amefanya mkutano wa hadhara katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Mara na kuzungumzia mpango wa Serikali kufanya uwekezaji mkubwa wa miundombinu ili kuibadilisha Manispaa ya Musoma.

Akiwahutubia wananchi wa Musoma, Mhe Simbachawene amesema katika mipango yake Serikali inampango wa kupanua treni ya kisasa ya SGR ifike Musoma, kujenga bandari kubwa na uwanja wa ndege wa kimataifa na miradi hii ikikamilika itaibadilisha kabisa Manispaa ya Musoma.

“Miradi hii haitafanywa kwa pamoja itafanywa kwa awamu ya miaka mitano mitano ili kuvutia watalii zaidi kuingia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuimarisha uchumi wa Mkoa wa Mara kwa kuufugua mkoa huu katika sekta ya usafirishaji” amesema Mhe. Simbachawene.

Akizungumzia kuhusu treni ya SGR, Mhe. Simbachawene amesema mpango wa Serikali baada ya treni hiyo kufika Mwanza, kutakuwa na mradi mwingine wa kujenga treni hiyo kuja Musoma na  itaunganishwa kuelekea Kenya, lengo likiwa ni kurahisisha usafirishaji wa  mizigo ambayo itapunguza bei za bidhaa baada ya kufika Musoma.

Mhe. Simbachawene amesema Serikali pia inampango wa kupanua na kuimarisha Bandari ya Musoma ili kuvutia meli kubwa kuweza kuta nanga katika bandari hiyo na kuimarisha usafirishaji wa mizigo na abiria na uchumi wa Manispaa ya Musoma.

Mhe. Simbachawene amesema Serikali inampango wa kujenga uwanja wa ndege wa Kimataifa baada ya kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa uwanja uliopo ili kuwavutia watalii wengi zaidi kuingia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa kupitia uwanja huo wa Musoma.

Mhe. Simbachawene amesema kwa sasa Mkoa wa Mara umekuwa ukipokea watalii wengi wanaoingia katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti baada ya kutambua kuwa ni rahisi kuingia ukitokea Wilaya za Bunda na Serengeti.

Mhe. Simbachawene amesema ndani ya miaka mitatu Mkoa umepata fedha nyingi kutokana na ongezeko la watalii kuliko wakati mwingine wowote.

Wakati huo huo, Mhe. Simbachawene amewataka vijana kutokuyumbishwa na watu wasiopenda maendeleo na badala yake kuchukua fursa hiyo kufuatilia mambo yanayofanywa na Serikali na taasisi zake katika kuwaletea wananchi huduma mbalimbali za maendeleo.

Mhe. Simbachawene amesema kwa kasi ya maendeleo inayofanyika hapa nchini, amani na utulivu ukiendelea kwa miaka mingine 25, Tanzania itakuwa imepiga hatua kubwa sana katika maendeleo ya kiuchumi, hivyo amewataka vijana kuilinda amani kwa nguvu zao zote.

Aidha, amewataka vijana kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 na Serikali Kuu wa mwaka 2025 ili kuwachagua viongozi bora wanaopenda maendeleo kuanzia kwenye mitaa, vijiji na vitongoji vyao hadi Taifa.

 Ziara ya Mhe. Simbachawene inatarajiwa kuendelea kesho katika Wilaya za Rorya na Tarime na tarehe 3 Oktoba, 2024 katika Wilaya ya Serengeti na Butiama na kuhitimishwa tarehe 4 Oktoba, 2024 katika Wilaya ya Bunda.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa