• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC ataka usimamizi thabiti wa Lishe Mara

Posted on: February 10th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Mungiya Mzee leo ameongoza kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa kipindi cha Julai-Desemba, 2022 na kuwataka viongozi na watendaji wa Serikali kusimamia kwa weledi utekelezaji wa afua za lishe kwenye maeneo yao.

Akizungumza katika kikao hicho, Mheshimiwa Mzee amewataka viongozi kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani ili Halmashauri ziweze kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya masuala ya lishe na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi katika utekelezaji wa mkataba wa lishe na kuepuka kuwa sehemu ya kuchochea changamoto hizo. 

“Viongozi tujitahidi kuhakikisha tunatekeleza Maagizo ya Serikali kuhusu mkataba wa lishe na kuacha kutoa visingizio mbalimbali kwa nini mkataba huo hautekelezeki” amesema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee amesema wanafunzi kula shuleni ni Maagizo ya Serikali, Wilaya na Halmashauri zihakikishe kuwa watoto wanapata angalau mlo mmoja shuleni kila siku ili kuwafanya wasome kwa ufanisi.

Aidha, Mheshimiwa Mzee amesema ataendelea kuchukua hatua kwa Wakurugenzi wa Halmashauri na viongozi wengine wote watakaokwamisha utekelezaji wa mkataba wa lishe katika maeneo yao bila sababu za msingi.

Mheshimiwa Mzee amesema hatakubali kuona Mkoa wa Mara unaendelea kuwa wa mwisho katika upimaji wa utekelezaji wa afua za lishe Kitaifa kutokana na uzembe wa viongozi na watendaji wenye dhamana ya kufanya hivyo.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewataka Wakuu wa Wilaya kuwasimamia watendaji wa Halmashauri zilizopo chini yao kuhakikisha chakula kinatolewa katika shule zote za msingi na sekondari ili watoto waweze kujifunza kwa ufanisi wakati wa masomo.

“Pamoja na kuwa kuna changamoto ya wazazi kutopenda kuchangia chakula au kutotaka watoto wao kula nje ya nyumba zao, viongozi mpo, tuwaelimishe hawa wazazi, inawezekana” amesema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, ameagiza shule zote katika Mkoa wa Mara kuacha mara moja utaratibu wa kuwaruhusu wauzaji wa vitu mbalimbali na badala yake kila shule iwe na jiko la kupika chakula cha wanafunzi ili kulinda afya za wanafunzi na walimu katika maeneo hayo.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Dkt. Zabron Masatu ameeleza kuwa kuwapa wanafunzi chakula wakiwa shuleni ni muhimu kwani linamanufaa makubwa katika ufundishaji na ujifunzaji wa watoto.

“Maeneo mengi imebainika kuwa wanafunzi wakipewa chakula hata mahudhurio ya watoto darasani yanaongezeka na wanaweza kusoma kwa ufanisi kuliko wakisoma na njaa” alisema Dkt. Masatu.

Aidha, alifafanua kuwa mwongozo wa chakula shuleni ni wa kitaifa na unatekelezwa na Halmashauri zote hapa nchini na katika Mkoa wa Njombe shule zote za msingi na sekondari wanatoa chakula na matokeo ya mitihani ya Kitaifa Mkoa huo unafanya vizuri na moja ya sababu ni kuwa wanafunzi wanapata chakula shuleni.  

Kikao cha tathmini ya lishe kimkoa kilihudhuriwa pia na Wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Idara na Vitengo vilivyopo ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Idara za Fedha, Mipango, Utawala na Rasilimali Watu, Waganga Wakuu wa Halmashauri na Maafisa Lishe.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Kusaya apokea vifaa vya mapambano dhidi ya HIV/UKIMWI

    May 06, 2025
  • Mtambi ataka elimu zaidi kutunza Maeneo ya Urithi wa Dunia

    May 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa