• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC aomba jeshi kuwekeza zaidi Mara

Posted on: January 11th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee amemuaomba Mkuu wa Majeshi Jenerali Jacob John Mkunda kuangalia uwezekano wa Jeshi la Tanzania kuwekeza zaidi katika shughuli za uzalishaji mali katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mzee ametoa ombi hilo wakati akimkaribisha Jenerali Mkunda aliyetembelea ofisini kwake wakati wa ziara yake ya kujitambulisha katika Vikosi vya jeshi vilivyomo katika Mkoa wa Mara na kuomba Jeshi liwekeze kwenye kilimo cha umwagiliaji na ufugaji waa samaki.

“Mkoa wa Mara tuna eneo kubwa linalopakana na Ziwa Victoria na mito lakini hamna kilimo cha umwagiliaji na hata ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba unafanywa kwa sehemu kubwa na jeshi tu, wananchi hawajapata elimu hiyo” alisema Mheshimiwa Mzee.  

Amelipongeza Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa kuwekeza katika ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba lakini ameliomba kuongeza zaidi uwekezaji na kuwafundisha wananchi wa Mkoa wa Mara kuhusiana na ufugaji wa samaki wa kitaalamu ili kuongeza uzalishaji katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa pamoja na mvua na uwepo wa Ziwa Victoria katika Mkoa wa Mara, hamna kilimo cha umwagiliaji na wakulima wengi hata wanaoishi kando kando ya ziwa wanalima kwa kutegemea mvua tu jambo ambalo alisema halileti tija.

“Hawa wananchi pamoja na elimu, lakini wanahitaji zaidi mfano waone jinsi kilimo cha umwagiliaji kinavyofayika na watapata nafasi ya kuiga jambo ambalo linaweza kukuza uchumi wao mmoja mmoja na Mkoa kwa ujumla” alisema Mheshimiwa Mzee.  

Aidha, Mkuu wa Mkoa ameliomba Jeshi kusaidia katika kukabiliana na uvamizi wa wavuvi katika Ziwa Victoria unaofanywa na wavamizi kutoka nchi Jirani za Kenya na Uganda jambo ambalo amesema linahatarisha maisha na kuwapa umaskini wavuvi wa Tanzania.  

Kwa upande wake Jenerali Mkunda ameshukuru kwa mapokezi mazuri aliyoyapata na kuahidi kuangalia uwezekano wa Jeshi kuwekeza zaidi katika Mkoa wa Mara.  

Jenerali Mkunda amemtaka Mkuu wa Mkoa kumtumia Mkuu wa Brigedi ya Magharibi yenye Makao Makuu yake katika Mkoa wa Tabora kufanikisha mipango mbalimbali ya maendeleo inayohitaji kufanywa na Jeshi katika Mkoa wa Mara.

Mkuu wa Majeshi amemahidi kuwa Jeshi litaendelea kulifuatilia kwa ukaribu tatizo la uvamizi wa wavuvi katika Ziwa Victoria ili kuweza kuchukua hatua stahiki kukomesha vitendo hivyo.

Aidha, amempongeza Mheshimiwa Mzee na viongozi wote wa Mkoa wa Mara kwa jitihada zinazoendelea kuchukuliwa kukabiliana na mila potofu ya ukeketaji wa wanawake katika Mkoa wa Mara.

Hii ni mara ya kwanza Jenerali Mkunda kutembelea Mkoa wa Mara tangu alipoteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Mkuu wa Majeshi ya Tanzania Juni, 2022.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa