• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC akagua uandikishaji wa wapiga kura Butiama

Posted on: October 15th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Mtambi leo amefanya ziara katika Wilaya ya Butiama kufuatilia maendeleo ya uandikishaji katika daftari la mkazi kwa ajili ya  maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mtaa na kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha ili kuweza kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Akizungumza na wananchi katika vituo hivyo, Mhe. Mtambi amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha pia washiriki katika kugombea nafasi mbalimbali zinazoshindaniwa katika uchaguzi huo.

“Tuitumie fursa hii ya kikatiba vizuri ili kuwachagua viongozi wanaofaa ili waweze kusimamia miradi ya maendeleo na kushughulikia kero zetu katika maeneo yetu” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi ametumia nafasi hiyo kuwapongeza wananchi wa Wilaya ya Butiama kwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuongeza kuwa kwa mwitikio uliopo anamatumaini kuwa Wilaya hiyo itafanya vizuri sana katika zoezi la uandikishaji.

Mhe. Mtambi pia amewataka wasimamizi wa uchaguzi kusimamia sheria, kanuni na taratibu lakini kama kuna changamoto zinazojitokeza kuhusiana na uchaguzi wazishughulikie mara moja ili kuondoa sintofahamu wakati huu wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Kwa upande wake, Bwana Nassoro Swaibu mkazi wa Kitongoji chaKitanga, Kijiji cha Butiama amempongeza Mkuu wa Mkoa kwa kukitembelea kitongoji hicho kwa ajili ya kuwahamasisha kuwachagua viongozi.

Bwana Swaibu amesema wananchi wengi wamehamasika na wanategemea kushiriki katika uchaguzi kutokana na hamasa iliyopo na ushirikiano baina ya viongozi katika Wilaya ya Butiama.

Kwa upande wake, Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi katika Jimbo la Butiama Bwana Gosbert Bernard amesema jimbo hilo linategemea kuandikisha wapiga kura 183,855 na hadi tarehe 14 Oktoba, 2024 tayari watu waliojiandikisha wamefikia 53,048 ambao ni sawa na asilimia 38.8.

Bwana Bernard amesema katika Jimbo la Butiama, mawakala wa vyama viwili vya siasa wameapishwa kwa ajili ya kusimamia uandikishaji ambavyo ni Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hata hivyo wanaosimamia zoezi kwenye vituo mpaka sasa ni mawakala wa CCM pekee.

Bwana Benard amesema mpaka sasa jimbo hilo halijapokea changamoto au malalamiko yoyote kutoka kwa wadau wa  uchaguzi au wananchi wa Wilaya ya Butiama na kuahidi kuzifanyia kazi changamoto zozote kwa kadiri zitakavyojitokeza.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa amefanya kikao cha ndani na viongozi na maafisa wanaohusika na usimamizi wa zoezi la uchaguzi kabla ya kuvitembelea vituo vya uchaguzi na kuzungumza na wasimamizi wa vituo na wananchi waliokuwepo kwenye vituo vya kuandikisha wapiga kura.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Butiama, baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Usalama Wilaya ya Butiama, baadhi ya maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.

Zoezi la uandikishaji wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa limeanza tarehe 11 Oktoba, 2024 na linatarajiwa kukamilika tarehe 20 Oktoba, 2024 na uchaguzi wa Serikali za Mitaa unatarajiwa kufanyika tatere 27 Novemba, 2024.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Maambukizi ya UKIMWI katika Wilaya ya Bunda yamepungua

    August 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa