• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC akabidhi zawadi ya Rais Samia Masanga

Posted on: December 26th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo tarehe 24 Desemba, 2022 amekabidhi zawadi za sikukuu kwa wahanga wa ukatili wanaoishi katika Kituo cha ATFGM Masanga Wilayani Tarime zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi hizo, Mheshimiwa Mzee amemshukuru sana Rais Samia kwa kuwakumbuka wahanga wa ukatili wanaoishi katika kituo hicho na kuwataka wahanga hao kuendelea kumuombea Rais Samia afya njema ili aendelee kuwahudumia Watanzania.

“Mheshimiwa Rais amenituma kuwaletea mkono wa kheri (zawadi) kwa ajili ya sikukuu zilizo mbele yetu za Krismasi na Mwaka Mpya” alisema Mheshimiwa Mzee na kumshukuru Rais kwa kitendo chake cha kutoa zawadi za sikukuu kwa vituo vingi hapa nchini.

Akiwa katika kituo hicho, Mheshimiwa Mzee amekemea wananchi wanaofanya vitendo vya ukatili kwa watoto wadogo  wasio na hatia kwa kisingizio cha mila zilizopitwa na wakati na kusema ukatili huo hauna tija kwa maendeleo ya wananchi wa Mkoa wa Mara.  

Mheshimiwa Mzee ametumia nafasi hiyo kuupongeza uongozi wa kituo hicho kwa jitihada za kuwasaidia watoto wanaokimbia majumbani mwao kutokana na vitendo vya ukatili hususan ukeketaji na ndoa za utotoni.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara Mheshimiwa Patrick Chandi Marwa ameeleza kuwa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara kinaunga mkono juhudi zinazofanywa na wadau mbalimbali kuwatunza wahanga wa ukatili katika jamii.

“Sisi kama Chama tutakemea na kuishauri vizuri Serikali kuhusu hatua za kuchukua ili kukomesha ukatili kwa mabinti unaotokana na ndoa za utotoni na ukeketaji” alisema Mheshimiwa Chandi.

Akizungumzia zawadi iliyotolewa, Mheshimiwa Chandi ameeleza kuwa Mheshimiwa Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ametoa zawadi kwa watoto hao kwa kuwa yeye na chama chake kinapinga vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto wakike.

Mheshimiwa Chandi amesema Mama Samia ametoa mbuzi 7, maharage kilo 80, mafuta na viungo mbalimbali na mchele kilo 450 kwa ajili ya wahanga hao kwa kuwa yeye kama Mama anafahamu madhara wanayoyapata watoto hao.

“Mheshimiwa Rais atakapokuja tena katika Mkoa wa Mara nitamuomba aje kutembelea kituo hiki ili kujionea mwenyewe kazi kubwa inayofanyika hapa. 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tarime Kanali Michael Mtenjele ameeleza kuwa Serikali imekua ikichukua hatua mbalimbali ili kuhakikisha inakomesha suala la ukeketaji lakini wananchi wamekuwa wakibuni mbinu mpya kila wakati kuendelea kufanya ukeketaji.

Mheshimiwa Mtenjele ameeleza kuwa mwaka huu umejitokeza ukatili mwingine kwa watoto wa kiume ambao baada ya kufanyiwa tohara salama hospitali watoto hao wanalazimishwa kupelekwa tena kwa ngariba na kufanyiwa tohara tena ya kimila.

“Jambo hili kimsingi ni ukatili wa aina yake, tumelikemea kwa nguvu zetu zote na polisi wamekuwa wakichukua hatua wanapopata taarifa za tohara hizo za kurudia na wananchi wameanza kuelewa hiyo changamoto haipo tena” alisema Kanali Mtenjele.

Aidha, Mheshimiwa Mtenjele amekishukuru sana Kituo cha AFTGM Masanga kwa msaada wanaoutoa kwa wahanga hao na hasa kwa watoto waliopo katika hatari ya kuingia kwenye ukeketaji.

Kwa upande wake Mkuu wa Kituo hicho Sista Jacqueline Gbanga Ya Bongo ameeleza kuwa kituo hicho kilianza mwaka 2008 baada ya watoto na wazazi ambao hawakupenda watoto wao kukeketwa kukimbilia katika nyumba ya watawa wa Kanisa Katoliki katika eneo hilo kwa ajili ya kuomba hifadhi.

Baadaye wazazi na mabinti waliendelea kuongezeka na hivyo wakaamua kuanzisha kambi kwa ajili yao na Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma likaanzisha Kituo hiki kwa ajili ya kuwahifadhi watoto na wazazi wanaokimbia.

Ameeleza kuwa tangu kuanzishwa kwa kituo hicho kimefanikia kuwaokoa watoto 4,392 waliopita katika kituo hicho kwa nyakati tofauti tofauti.

“Kwa mwaka 2022, kituo hiki kimepokea watoto 486 na baadhi ya watoto hao tayari wameanza kuwarudisha nyumbani kwao baada ya kuzungumza na wazazi na viongozi wa vijiji na kuhakikishiwa usalama wa watoto hao baada ya kurejea majumbani kwao” alisema Sista Jacqueline.

Mkuu huyo wa Kituo ameishukuru sana Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushirikiano mkubwa sana wanaoutoa katika Kituo cha Masanga na amemshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kutoa zawadi hizo ambazo ameeleza zitawasaidia watoto hao kupata chakula wakati huu wa sikukuu. 

Katika ziara hiyo, RC aliongozana pia na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu, baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Mkoa, Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Mkoa na watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wilaya na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa