• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC aitaka NDC kuwa Balozi wa Mkoa wa Mara

Posted on: January 13th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amelipokea kundi la viongozi, wakufunzi, maafisa na wanachuo kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) waliopo Mkoani Mara katika ziara ya mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa kozi ya 13 ya Chuo hicho na kuwataka wageni hao kuwa mabalozi wa Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika hafla ya mapokezi ya ugeni huo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji, Mhe. Mtambi amewataka viongozi, maafisa na wanachuo hao kuyatangaza mambo mazuri watakayoyaona katika Mkoa wa Mara na hususan katika sekta watazitembelea katika ziara hiyo.  

“Mkoa wa Mara una mambo mengi mazuri na fursa nyingi za kiuchumi katika sekta za utalii, madini, kilimo, viwanda na biashara” na kuongeza kuwa “Mara ina kapeti la dhahabu, kuna migodi ya madini katika Wilaya zote sita za Mkoa wa Mara” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewataka wageni hao kuhakikisha wanapata nyama choma na kichuri ili kuonja radha tamu ya nyama za Mkoa wa Mara na kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kujionea uzuri wa hifadhi hiyo inayopatikana katika Mkoa wa Mara.  

Mhe. Mtambi amesema kundi lililopo katika Mkoa wa Mara litatembelea Wilaya za Butiama, Tarime, Musoma na Serengeti na litapita katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, kumbukumbu na historia, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mheshimiwa Mtambi amewataka wanachuo na wakufunzi hao kufanyia upembuzi masuala ya kiutamaduni, kisiasa, kijamii na kiuchumi na kutoa mapendekezo wakati wa kuhitimisha ziara hiyo ya mafunzo katika Mkoa wa Mara.   

Mhe. Mtambi amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kutoa ushirikiano kwa kuwapokea na kuwapa msaada na taarifa zinazohitajika ambapo wanatarajiwa kuwepo kwa muda wa siku tano kuanzia leo tarehe 13 Januari, 2025 hadi tarehe 18 Januari, 2025.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Chuo Taifa cha Ulinzi (NDC) Meja Jenerali Balozi Wilbert Augustin Ibuge amesema Chuo hicho kinatoa mafunzo mbalimbali ya muda mrefu na mafunzo ya muda mfupi kulingana na mahitaji ya Taasisi mbalimbali wao.

Meja Jenerali Ibuge ameeleza kuwa katika mwaka wa masomo 2024/2025 Chuo hicho kina wanachuo 61 wa kundi la 13 ambao walianza mafunzo ya darasani Septemba, 2024 na wanatarajiwa kukamilisha mafunzo yao Julai, 2025 na kati yao wanachuo 41 wanatoka Tanzania na wanachuo 15 wanatoka katika mataifa rafiki.

Mhe. Ibuge amesema, jumla ya wanachuo wakiwemo watanzania 10 na wanafunzi kutoka nchi nyingine watano wamefika Mkoa wa Mara kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo na kueleza kuwa lengo la ziara hiyo ni kujifunza kuhusu utekelezaji wa Sera za Taifa uwandani katika sekta mbalimbali.

Meja Jenerali Ibuge ambaye pia aliwahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amesema katika awamu hii mikoa iliyotembelewa na makundi ya wanachuo hao ni pamoja na Mara, Kagera, Ruvuma. Mtwara, Katavi, Songwe, Pwani na Morogoro.  

Chuo cha Taifa cha Ulinzi kilianzishwa rasmi mwaka 2011 na kilizinduliwa rasmi Septemba, 2012 na makao makuu yake yakiwa Jijini Dar es Salaam.   

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Kusaya apokea vifaa vya mapambano dhidi ya HIV/UKIMWI

    May 06, 2025
  • Mtambi ataka elimu zaidi kutunza Maeneo ya Urithi wa Dunia

    May 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa