• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC afanya ziara Wilaya ya Musoma

Posted on: August 18th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Sulaiman Mzee leo tarehe 16 Agosti, 2022 amefanya ziara ya kujitambulisha katika Wilaya ya Musoma na kuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kuwasilisha maelezo ofisini kwake kwa nini miradi ya ujenzi imesimama.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi wa ofisi za Halmashauri na Hospitali ya Hamashauri ya Wilaya ya Musoma, Mheshimiwa Mzee ameutaka uongozi ya Halmashauri hiyo kuwa kutoa maelezo ya kina kwa nini miradi hiyo.

“Ninataka maelezo ya kina kwa nini miradi hii imesimama na fedha za ujenzi wa miradi hii zipo kwa muda mrefu lakini ujenzi hauendelei na wala haujakamilika” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee aliagiza kuchukuliwa hatua za kisheria kwa wahusika wote wa ujenzi wa jengo la Halmashauri baada ya kupewa taarifa kuwa kutokana na upotevu wa nondo 1,026 katika mradi huo, maafisa wote waliowekwa ndani wamepewa dhamana na Mtunza Stoo tu ndiye anashikiliwa na polisi.

Mkuu wa Mkoa aliagiza Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kuendelea kukamilisha miradi hiyo kwa haraka ili wananchi waweze kupata huduma inayostahili.

Kwa Upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bwana Msongela Nitu Palela ameeleza kuwa miradi hiyo imesimama kutokana na uchunguzi unaofanyika kufuatia wizi wa nondo kubainika katika mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi za Halmashauri hiyo.

“Tumeunda tume ambayo inafanyakazi kwa siku tatu kukagua vifaa vyote vilivyoko kwenye stoo ili kujiridhisha baada ya kubaini wizi huo wa nondo katika mradi wa ujenzi wa ofisi za Halmashauri” amesema Palela.

Bwana Palela ameeleza kuwa kwa sasa miradi yote imesimama kufuatia uchunguzi unaoendelea na kukosekana kwa mtaalamu wa stoo ambaye anashikiliwa na Jeshi la Polisi kufuatia wizi huo.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Mzee ametembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Musoma na baadaye miradi ya ujenzi ya ofisi za Halmashauri na Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya, ofisi za Chama cha Mapinduzi (CCM) Musoma vijijini na jengo jipya la CCM linalojengwa Musoma vijijini.

Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu, Mkuu wa Wilaya ya Musoma, viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Musoma na viongozi wengine wa CCM wa Wilaya ya Musoma.

 Huu ni mwendelezo wa ziara za Mkuu wa Mkoa tangu alipoteuliwa kuja Mara na kuanza kazi tarehe 6 Agosti, 2022.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mara kuwawezesha wanawake kiuchumi kupunguza ukatili

    June 30, 2025
  • Mtambi afungua kambi ya madaktari bingwa na bobezi 64 Mara

    June 23, 2025
  • Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara wapatiwa mafunzo

    June 20, 2025
  • Mara mshindi wa pili UMITASHUMTA 2025

    June 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa