• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Rais Samia atoa milioni 100 kusaidia maafa Musoma

Posted on: March 26th, 2025

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo ametoa shilingi milioni  mia moja (100,000,000) kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa mvua na upepo mkali uliotokea katika Kata 10 za Manispaa ya Musoma tarehe 23 Machi, 2025.

Msaada huo umekabidhiwa leo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi na Mshauri wa Kisiasa wa Mhe. Rais Mhe. Haji Omar Kheir (Mb.) aliyewasili Musoma leo tarehe 26 Machi, 2025 kufuatia maafa hayo.   

Akizungumza na wananchi katika maeneo mbalimbali amesema Mhe. Rais anawashukuru sana wananchi wa Musoma kwa ustahimilivu wao kufuatia maafa hayo na kuwataka kuendelea kuwa na utulivu wakati Serikali ikiendelea kutatua changamoto hiyo iliyojitokeza.

Mhe. Kheir amesema baada ya kupokea taarifa za maafa hayo, Mhe. Rais alitoa maelekezo mahususi ya namna ya kushughulikia maafa hayo na amewatuma washauri wake wa kisiasa kuja kufanya tathmini na kumjulisha hali halisi ya maafa hayo.

Wakati huo huo, Washauri wa Kisiasa wa Mhe. Rais leo wakiwa wanazungumza na waathirika katika kambi maalum ya waathirika hao wamechangia shilingi 3,500,000.00 kwa ajili ya kuwasaidia wathirika wa tukio hilo.

Fedha hizo zimetolewa na Mhe. Mhe. Kheir shilingi 2,000,000.00,  Mhe. Alhaj Abdalla Bulembo shilingi 1,000,000.00 na Mhe. Balozi Rajab Omar Luhwavi shilingi 500,000.00

Aidha, Mbunge wa Jimbo la Musoma Mhe. Vedastus Mathayo ametoa mitungi mikubwa miwili ya gesi na majiko yake kwa ajili ya kupikia katika kambi hiyo na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara Mhe. Ghati Chomete amechangia mchele kilo 100.   

Akizungumza katika makabidhiano ya pesa hizo, Mhe. Mtambi amesema wananchi wa Mkoa wa Mara wamefarijika sana kwa moyo wa ukarimu na upendo kwa wananchi aliouonyesha tangu maafa yalipotokea katika Mkoa wa Mara.

Mhe. Mtambi ameahidi kuwa fedha hizo na nyingine zitakazotolewa zitatumika vizuri katika kutoa huduma kwa waathirika na kurejesha maisha ya wananchi katika hali ya awali.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara Mhe. Patrick Chandi Marwa amemshukuru Mhe. Rais kwa msaada wa haraka alioutoa kwa waathirika wa maafa hayo na kuongeza kuwa wananchi wa Mkoa wa Mara wanafarijika sana na msaada huo.

Mhe. Chandi amewataka wadau mbalimbali wa maendeleo kujitokeza na kutoa msaada kwa wananchi walioathirika na tukio hilo ili waweze kurejea katika hali zao za awali mapema iwezekanavyo.

Mhe. Chandi ameipongeza Serikali ya Mkoa kwa kuwasaidia wananchi kwa haraka na kuwatafutia makazi ya muda wakati jitihada za kuwarejesha katika maeneo yao ya awali zikiendelea.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa