• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mwenge wa Uhuru kupitia miradi ya bilioni 24.96 Mara

Posted on: July 25th, 2024

MWENGE WA UHURU KUPITIA MIRADI YA BILIONI 24.96 MARA

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ofisini kwake ametoa taarifa kwa Waandishi wa Habari kuhusu maandalizi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2024 katika Mkoa wa Mara mapokezi yake yanayotarajiwa kufanyika kesho katika uwanja wa Shule ya Msingi Robanda, Wilaya ya Serengeti.  

Mhe. Mtambi amesema Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka huu zitapita katika miradi ya maendeleo 72 yenye thamani ya shilingi 24,961,723,115.48 iliyotekelezwa kwa michango ya wananchi, Halmashauri, Serikali Kuu na wahisani.

“Miradi itakayotembelewa ipo katika sekta za elimu, kilimo, ujenzi, maji, afya, mifugo, mazingira, ustawi wa Jamii, viwanda na biashara na shughuli za vijana” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema maandalizi ya kupokea Mbio za Mwenge wa Uhuru yamekamilika na ukiwa katika Mkoa wa Mara utakimbizwa katika Wilaya sita na Halmashauri tisa katika umbali wa kilomita 1,037.80.

Kanali Mtambi amesema ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu ni kuhusu utunzaji wa mazingira na uchaguzi wa Serikali za Mitaa chini ya kauli mbiu: Tunza Mazingira na shiriki Uchaguzi wa Serikali za mitaa kwa ujenzi wa Taifa Endelevu.

Akizungumzia ratiba ya Mbio za Mwenge wa Uhuru, Kanali Mtambi amesema Mwenge unatarajiwa kukimbizwa kuanzia Serengeti tarehe 26/ 7/ 2024,   Tarime DC tarehe 27/7/2024, Tarime TC tarehe 28/7/2024, Rorya 29/7/2024 na Manispaa ya Musoma tarehe 30/7/2024.

Mwenge utakimbizwa Musoma DC tarehe 31/7/2024, Butiama tarehe 1/8/2024, Bunda DC tarehe 2/8/2024,  Bunda TC tarehe 3/8/2024 na tarehe 4/8/ 2024 Mwenge utakabidhiwa katika Mkoa wa Simiyu kuendelea na mbio zake.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara amewakaribisha viongozi, watendaji na wananchi wote kushiriki katika maadhimisho ya miaka 60 ya Mwenge wa Mwitongo yatakayofanyika nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mwitongo tarehe 1 Agosti, 2024.

Mwenge wa Mwitongo ni mwenge wa Kabila la Wazanaki ambao upo Nyumbani kwa Baba wa Taifa na unawashwa kila mwaka Mbio za Mwenge wa Uhuru zikiwa katika Mkoa wa Mara tangu mbio hizo zilipoanzishwa mwaka 1964.

Mhe. Mtambi amesema mwaka huu ni mwaka maalum kwa Mbio za Mwenge wa Uhuru ambapo unaadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, miaka 60 ya Muungano wa Tanzania na Miaka 60 ya Mbio za Mwenge wa Uhuru.

Mhe. Mtambi amewashukuru wananchi wa Mkoa wa Mara ambao wamechangia kwa hali na mali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na hususan itakayotembelewa na Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu.

Mhe. Mtambi amewataka wananchi wote kushiriki mbio, mapokezi, mikesha na shamrashamra za Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Kusaya apokea vifaa vya mapambano dhidi ya HIV/UKIMWI

    May 06, 2025
  • Mtambi ataka elimu zaidi kutunza Maeneo ya Urithi wa Dunia

    May 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa