• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtanda amtaka Mkandarasi kukamilisha ujenzi wa soko- Tarime

Posted on: October 24th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohammed Mtanda leo amefanya ziara katika Wilaya ya Tarime na kumtaka Mkandarasi wa Soko la kimkakati la Halmashauri wa Mji  wa Tarime kukamilisha mradi huo kwa mujibu wa mkataba tarehe 18 Novemba, 2023.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa Serikali imeleta pesa yote ya utekeleaji wa mradi huo hata hivyo Mkandarasi wa mradi huo Mohammed Builders Limited ndie anayechelewesha ukamilishaji wa mradi huo huku wananchi wakisubiria huduma.

“Mkandarasi aagizwe kuongeza watumishi na aanze kukamilisha kazi za nje na maduka ya nje ya soko hili ili yaanze kutoa huduma kwa wananchi na hamna muda utakaoongezwa tena katika mkataba wake”  amesema Mhe. Mtanda.

Aidha amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri wa ya Mji wa Tarime kutenga maeneo ya wafanyabiashara wadogo, pikipiki na bajaji na mama/baba lishe katika soko hilo ili wateja wa hali zote waweze kuhudumiwa na soko hilo.

Aidha, amemuagiza Mhandisi Mshauri kuwasilisha ofisini kwake nakala ya ushauri na mapendekezo aliyoyatoa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Tarime kuhusiana na ujenzi wa soko hilo.

Mhe. Mtanda amezitaka Halmashauri nyingine za Mji wa Bunda na Manispaa ya Musoma kuiga ubunifu wa Halmashauri ya Mji wa Tarime kwa uwekezaji huo ambao amesema utawanufaisha wananchi na wafanyabiashara wa Mji wa Tarime.  

Akitoa taarifa ya mradi, Mhandisi Mshauri Eng. Leonard Mwangoka ameeleza kuwa mradi huo wenye thamani ya shilingi bilioni 9.5 ulipangwa kukamilika ndani ya miezi 15 kuanzia tarehe 19 Januari, 2022 hadi tarehe 19 Aprili, 2023 hata hivyo Mkandarasi ameongezewa muda hadi tarehe 18 Novemba, 2023.

Eng. Mwangoka ameeleza kuwa mradi kwa sasa upo katika hatua ya ukamilishaji wa mradi huo na ujenzi unaendelea vizuri na unakadiriwa kufikia asilimia 84 ya utekelezaji wake.

“Kazi zinazoendelea ni ujenzi wa terrazzo katika maeneo ya vizimba na kolido zote, plasta baadhi ya maeneo, upakaji wa rangikatika maduka ya nje, kuweka milango kwenye maduka, uwekaji wa vizingiti vya chuma kwenye kolido na kuweka bodi za umeme kwenye maduka” amesema Mhandisi Mwangoka.

Bwana Mwangoka ameeleza kuwa mpaka sasa Mkandarasi wa mradi huo ameshalipwa zaidi ya shilingi 4.7 ambayo ni sawa na asilimia 49.9 ya malipo yote anayotakiwa kulipwa na kwa sasa malipo yaliyopo kwa mwajiri ni shilingi milioni moja tu.

Kwa mujibu wa Eng. Mwangoka, hadi kufikia tarehe 23 Oktoba, 2023 mradi huo umetoa ajira kwa watu 441 na utakapokamilika utakuwa na maduka ya nje 134, maduka ya ndani 188, vizimba 160, bucha 3, migahawa 2, supamaketi 1 na benki 2.

Akiwa katika Halmashauri ya Mji wa Tarime, Mkuu wa Mkoa alitembelea pia mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Nyagisese na kupongeza Halmashauri ya Mji wa Tarime kwa kazi nzuri iliyofanyika katika ujenzi wa shule hiyo.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Tarime, baadhi ya maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, baadhi ya viongozi na wataalamu wa Halmashauri ya Mji wa Tarime.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Chakula Shuleni Mkoa wa Mara ni Lazima- Kusaya

    September 02, 2025
  • Mwenge wa Uhuru Wapitisha miradi 68 ya bilioni 26.5 Mara

    August 23, 2025
  • RC Mtambi akutana na viongozi wa dini na kuwasistiza kuhamasisha amani

    August 22, 2025
  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa