• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi: Vifaa vya chanjo vitumike kwa makusudio stahiki

Posted on: January 24th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Afred Mtambi leo amekabidhi gari na pikipiki 15 ambazo zitatumika kwa ajili ya kusambaza chanjo katika Mkoa wa Mara na kuwataka wataalamu kuvitumia vifaa hivyo kwa kuzingatia malengo yaliyokusudiwa.

Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa hivyo, Mhe. Mtambi amesema gari na pikipiki hizo ni mpya na amezikagua zipo vizuri hivyo zikitumika vizuri kwa makusudi yaliyokusudiwa vinaweza kudumu na kutoa huduma kwa muda mrefu.

“Watumishi tutakaovitumia vifaa hivi tuhakikishe tunavitunza na kuvitumia kwa makusudio stahiki,  nivikagua vyote na nimeendesha gari hili, vifaa hivi ni vipya kabisana ni vya viwango vya hali ya juu, twendendi tukavitumie kwa makusudio stahiki” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi ametumia fursa hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo amekuwa akitujali watanzania kwa kutoa vifaa hivyo kwa ajili ya kurahisisha zoezi la chanjo katika Mkoa wa Mara.

Mhe. Mtambi amewataka wazazi kuwapeleka watoto kwenye chanjo na kuepuka imani potofu kuhusu baadhi ya chanjo zinazotolewa hapa nchini na kuwatahadharisha kuhusu umuhimu wa watoto kupata chanjo mapema ili kuweza kuwakinga na magonjwa mbalimbali.

Awali akitoa taarifa kuhusiana na vifaa hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya amesema gari na pikipiki hizo zimetolewa na Wizara ya Afya kwa ajili ya zoezi la chanjo katika Mkoa wa Mara.

Bwana Kusaya amesema gari hilo litatumiwa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa ajili ya kusambaza chanjo, wakati pikipiki 15 zimegawiwa kwenye Halmashauri zote kwa ajili ya matumizi ya wasimamizi wa chanjo na Halmashauri sita kati ya tisa zimepatiwa pikipiki mbili mbili.

Bwana Kusaya ameishukuru Wizara ya Afya kwa kutenga bajeti ya kuimarisha vitendea kazi kwa wataalamu wa afya na hususan vifaa hivyo ambavyo vimetolewa kwa ajili ya usimamizi wa zoezi la chanjo katika Mkoa wa Mara.

Gari la kusambaza chanjo limekabidhiwa kwa Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii wakati pikipiki zimekabidhiwa kwa Wakuu wa Wilaya kwa ajili ya kukabidhiwa Halmashauri mbalimbali zilizopo katika Mkoa wa Mara.

 Hafla ya kukabidhi vitendea kazi hivyo imehudhuriwa Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Wilaya, Menejimenti ya Sekretarieti ya Mkoa, Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Timu ya Usimamizi wa Sekta ya Afya Mkoa, Waganga Wakuu, Maafisa Lishe, Waweka Hazina, Maafisa Utumishi, Maafisa Elimu Msingi na Sekondari na Maafisa Mipango wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa