• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi: Mara haitamvumilia anayevuruga amani iliyopo

Posted on: March 1st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 01 Machi, 2025 ameongoza hafla ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara kuwatunuku askari waliofanyakazi nzuri kwa mwaka 2024 iliyofanyika katika viwanja vya Field Force, Manispaa ya Musoma ambapo amewataka wanasiasa wa Mkoa wa Mara kufanya siasa zao kwa kuzingatia amani na utulivu.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mtambi amesema Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara imejiandaa vizuri kwa ajili ya kusimamia amani na utulivu wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na haitamvumilia mtu yoyote anayefanya siasa potoshi, kutoa matamko yanayochochea uvunjifu wa amani na kuvuruga amani na utulivu uliopo katika Mkoa.

“Wale wote watakaopandwa na homa ya uchaguzi bila kujali vyama vyao vya siasa, Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara itawapa sindanao na dawa stahiki ili kushusha homa hiyo kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo” amesema Mhe. Mtambi na kuwahakikishia wanasisasa wanaopenda amani na utulivu kuwa watafanya shughuli zao katika mazingira salama.

Mhe. Mtambi amewataka watendaji wa vyombo vya ulinzi na usalama kuacha kujiingiza kwenye masuala ya kisiasa na kuwataka kufuata taratibu zinazowaruhusu kupiga kura na kuchagua viongozi mbalimbali wanatakaoshiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Kanali Mtambi amelipongeza Jeshi la Pilisi Mkoa wa Mara kwa kazi nzuri wanayoifanya na kuwapongeza askari wote waliopewa vyeti vya heshima na zawadi kwa kazi nzuri waliyoifanya na kuwataka kuendelea kufanyakazi na kuiishi kauli mbiu yao ya Nidhamu, Haki, Weledi na Uadilifu ili amani na usalama uliopo Mkoa wa Mara uendelee kutamalaki.  

Aidha, amewapongeza wananchi wa Mkoa wa Mara wanaotoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi na kuwataka wananchi wote kuendelea kutoa ushirikiano ili kuuweka Mkoa wa Mara kuwa ni sehemu salama kwa shughuli za uchumi na maendeleo na kuweza kuvutia wawekezaji na watalii zaidi.

Mhe. Mtambi amewapongeza wadau malimbali wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara ambao wamekuwa wakisaidia jitihada mbalimbali za jeshi hilo katika kusimamia amani na usalama wa wananchi na mali zao na kuwataka wadau hao kuendelea kuliunga mkono Jeshi la Polisi na kutoa ushirikiano.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (ASP) Pius Lutumo amesema zoezi la kuwatambua askari na wadau waliofanya vizuri lipo kwa mujibu wa taratibu za Jeshi hilo na taratibu za kawaida za Utumishi wa Umma.

ASP Lutumo amesema askari na wadau waliotunukiwa leo wamefanyakazi nzuri kwa Jeshi la Polisi katika mwaka 2024 na kuwa askari wote wamepewa vyeti na pesa taslimu shilingi 500,000 kila mmoja na kuwapongeza wote waliofanikiwa kutunukiwa zawadi hizo.

Kamanda Lutumo amesema utoaji wa zawadi hizi ni tafsiri ya Inspekta Generali wa Polisi (IGP) kuhusiana na maelekezo yanayotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kuhusiana na kuwapa askari mafunzo kazini,  motisha wanapofanyakazi nzuri na kuendelea kuwapunguza askari wanaolitia doa jeshi hilo.

Mhe. Mtambi akiwa katika hafla hiyo mbali na kuzungumza na askari, amekagua gwaride la heshima lililoandaliwa kwa ajili ya hafla hiyo, amewatunukia vyeti vya heshima na zawadi baadhi ya askari waliofanya vizuri na wadau wa Jeshi la Polisi Mara na kuangalia maonyesho ya vikosi mbalimbali vya Jeshi la Polisi.

Hafla hiyo imehudhuriwa na Kamati ya Amani na Maridhiano Mkoa wa Mara, wadau mbalimbali na askari pamoja na familia zao.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Maambukizi ya UKIMWI katika Wilaya ya Bunda yamepungua

    August 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa