• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi azipongeza Halmashauri kwa kupata hati safi

Posted on: April 29th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao cha kujadili maagizo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na kuzipongeza Halmashauri zilizopata hati safi katika ukaguzi wa hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtambi amesema Halmashauri nane za Mkoa wa Mara zimepata hati safi wakati Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ikiwa imepata hati isiyoridhisha katika ukaguzi wa CAG kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

“Ninawapongeza sana kwa kazi kubwa iliyofanywa na Halmashauri za Mkoa wa Mara katika kufunga hesabu za Serikali na kutoa ufafanuzi unaohitajika kwa wakaguzi wa hesabu za serikali” amesema Kanali Mtambi na kuitaka Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kuchukua hatua kurekebisha hati hiyo katika kaguzi zijazo.

Mhe. Mtambi ameelekeza Kamati za Fedha na Mipango za Halmashauri kuwachukulia hatua watumishi ambao kwa namna moja au nyingine walisababisha hoja za ukaguzi kutokana na uzembe na ofisi yake ipate taarifa ya hatua zilizochukuliwa kwa watumishi hao.

Mhe. Mtambi amezitaka Halmashauri kuyafanyia kazi maagizo yote ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC) na hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha 2022/2023 na hoja za miaka ya nyuma.  

Aidha, ameyataka Mabaraza ya Madiwani katika Halmashauri kusimamia matumizi ya fedha za wajibu wa migodi kwa jamii (CSR) ili miradi inayotekelezwa kwa fedha za CSR iweze kukamilika kwa wakati kwa kutumia bajeti iliyopangwa. 

Kanali Mtambi amezitaka Halmashauri kuendelea na maandalizi ya mbio za Mwenge wa Uhuru ambapo Mkoa wa Mara unategemea kupokea Mwenge wa Uhuru tarehe 26 Julai, 2024 hadi tarehe 3 Julai, 2024  na kuzitaka Halmashauri kutoa kipaumbele katika maandalizi ya mapokezi na Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2024.

Mtambi amezitaka Halmashauri kuacha kutumia fedha za makusanyo kabla ya kupelekwa Benki na kuzitaka kufuata miongozo, sheria, kanuni na taratibu za matumizi ya fedha za Serikali na kufanya usuluhishi wa mahesabu kabla ya tarehe 10 ya kila mwezi.

Mhe. Mtambi amewataka viongozi na watendaji wa Halmashauri kusikiliza na kutatua kero na changamoto zinazowakabili wananchi katika maeneo yao na kuratibu kero zilizotatuliwa katika kila ngazi ili kupata rejea inapoibuka tena sehemu nyingine.  

Kwa upande wake, akitoa taarifa katika kikao hicho Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Menejimenti ya Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi (MMI) Bwana Marco Maduhu ameeleza kuwa LAAC iliziita Halmashauri sita za Mkoa wa Mara kwenda Dodoma na kuzitembelea Halmashauri tatu ambazo hazikuitwa Dodoma na kutoa maagizo mbalimbali.

Bwana Maduhu ameeleza kuwa LAAC ilitoa jumla ya maagizo 45 kwa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara na kati ya hayo maagizo manne yamejibiwa, maagizo 21 yapo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na maagizo 20 hayajatekelezwa.

Kikao hicho kimehudhuriwa na waheshimiwa Wakuu wa Wilaya, Menejimenti ya Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala wa Wilaya, Kamati za Fedha za Halmashauri na Menejimenti zote za Halmashauri za Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa