• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi aunda kamati kushughulikia mgogoro Majimoto

Posted on: August 17th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 13 Agosti, 2024 amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Kata ya Majimoto kushughulikia mgogoro kati ya mgodi wa madini na wananchi na kuunda kamati itakayopitia na kufuatilia uhalisia wa taarifa za mgogoro huo na kutoa mapendekezo.

Akizungumza baada ya kukagua eneo la Mgodi wa Dhahabu wa Kahungwa Majimoto Mining na kusikiliza malalamiko ya wananchi kuhusiana na mgogoro huo, Mhe. Mtambi amesema kuwa timu hiyo itakayowahusisha viongozi, watendaji na walalamikaji itasaidia katika kuweka sawa baadhi ya taarifa zilizopo kabla ya kutoa maamuzi.

“Ninatoa wiki tatu kwa kamati hiyo kukamilisha kazi yake na kuwasilisha taarifa katika ofisi yangu ili niweze kufanya maamuzi kuhusiana na mgogoro huu” amesema Mhe. Mtambi na kuongeza kuwa Mkoa utafanya maamuzi na kuchukua hatua stahiki baada ya kupokea taarifa ya kamati hiyo.  

Mhe. Mtambi amesema kamati hiyo itakuwa na wajumbe kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Ofisi ya Afisa Madini Mkoa wa Mara, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na wawakilishi wa walalamikaji na mwekezaji katika mgogoro huo.

Hata hivyo, Mhe. Mtambi amewatahadharisha wananchi wanaotoa taarifa za uongo katika kukuza mgogoro huo na wananchi wanaoleta usumbufu usio na sababu kwa wawekezaji kwa kuwa Mkoa wa Mara utahakikisha wawekezaji katika Mkoa huo wanafanya kazi katika mazingira rafiki ya uwekezaji.

“Mkoa wa Mara hatutamvumilia mtu yoyote anayewavuruga wawekezaji kwa maslahi yake binafsi, tutachukua hatua kali kwa wale wote wanaochochea migogoro isiyo na misingi na wawekezaji” amesema Mhe. Mtambi.

Kwa upande wake akizungumza katika mkutano huo, Mbunge wa Serengeti Mhe. Dkt. Amsabi Mrimi amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kufika katika eneo hilo kuwasikiliza wananchi na kuunda kamati ya kushughulikia mgogoro huo.

Dkt. Mrimi amewapongeza wananchi wa eneo hilo kwa ustahimilivu katika mgogoro huo na kuwataka kuendelea hivyo ili suluhu yenye manufaa kwa mwekezaji na wananchi iweze kupatikana kwa kufuata sheria za nchi.

Mhe. Mrimi amewataka wananchi wa Majimoto kutoa ushirikiano kwa kamati hiyo na hususan kutoa taarifa sahihi ili kamati iweze kutekeleza majukumu yake kiufanisi na kupata muafaka wa mgogoro huo mapema iwezekanavyo.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Maambukizi ya UKIMWI katika Wilaya ya Bunda yamepungua

    August 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa