• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi akemea michakati isiyoisha kwenye miradi ya maendeleo

Posted on: April 13th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 11 Aprili, 2025 amefanya ziara katika Wilaya za Musoma na Tarime kwa lengo la kukagua miradi ya maendeleo na kuwakemea watendaji kuhusu michakato isiyoisha katika utekelezaji wa miradi.

Akizungumza kwa nyakati tofauti katika ziara hiyo, Mhe. Mtambi amewataka viongozi na watendaji wa Serikali kukamilisha miradi ya maendeleo kwa wakati ili miradi hiyo iweze kutoa huduma zilizopangwa kwa wananchi.

“Sitaki kusikia habari za michakato isiyoisha katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Mara, kamilisheni miradi ya maendeleo kwa wakati ili huduma zitolewe katika miradi hiyo” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema awali, tatizo lilikuwa upatikanaji wa fedha za utekelezaji wa miradi, kwa sasa Mheshimiwa Rais ameleta fedha za kutekeleza miradi lakini michakato inafanyika taratibu na kukwamisha utekelezaji wa miradi kwa wakati na kusababisha wananchi kukosa huduma inayotarajiwa na Mhe. Rais wakati analeta fedha.

Aidha, amewataka watendaji kuacha kutumia kisingizio cha ugumu wa matumizi ya mfumo wa Manunuzi Serikalini (NEST) baada ya kuchelewesha kukamilisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuwahakikishia kuwa mfumo upo vizuri na Halmashauri nyingine zinafanya vizuri katika matumizi ya mfumo huo.

Wakati huo huo, Mhe. Mtambi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wingi katika Mkoa wa Mara tangu alipoingia madarakani.

“Mkoa wa Mara tumependelewa kwa kupewa miradi mingi ya kimkakati, ambayo ikikamilika itaufanya Mkoa na wananchi wake kupiga hatua kubwa sana kimaendeleo” amesema Mhe. Mtambi.

Akiwa katika Wilaya ya Musoma, Mhe. Mtambi amekagua ukarabati na upanuzi wa Uwanja wa Ndege Musoma wakati akiwa Tarime ametembelea ujenzi wa Shule ya Sekondari Mpya ya Kibumaye na kutembelea na kuzungumza na wanafunzi wa Shule ya Msingi Mogabiri.

Aidha, Mhe. Mtambi amekagua na kutembelea mradi wa barabara ya Mogabiri- Nyamongo (KM 25) inayojengwa kwa kiwango cha lami ikiwa ni sehemu ya barabara ya Tarime- Mugumu, amekagua mradi wa upanuzi wa miundombinu katika Shule ya Sekondari ya Julius Kambarage Nyerere.

Mhe. Mtambi amehitimisha ziara yake kwa kumtembelea Mkandarasi mzawa Isack Charles Wange ambaye ni mmiliki wa RIN Contractors and General Supply Campany Limited ofisini kwake katika eneo la Nyamongo ambaye ni mdau muhimu wa maendeleo ya Wilaya ya Tarime.

Katika ziara hiyo, Mhe. Mtambi ameambatana na Wakuu wa Wilaya za Musoma na Tarime, Maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, TANROADS, TAA, Halmashauri ya Tarime na Wakandarasi na wazabuni wanaotekeleza miradi hiyo. 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa