• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa aagiza wazazi wa watoto 70 waliokeketwa wakamatwe

Posted on: January 11th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo tarehe 10/1/2023 ameliagiza Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Tarime/Rorya kuwakamata wazazi/walezi wa watoto 70 waliokuwa wamekimbilia AFTGM Masanga kukwepa ukeketaji na baadaye kurejeshwa kwa wazazi wao baada ya kipindi cha ukeketaji kupita.

Akizungumza katika nyumba salama zilizopo katika Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Mzee amelitaka Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara na Kanda Maalum ya Tarime/ Rorya kuwakamata viongozi wa Serikali za Vijiji na Mitaa ambamo mabinti hao walikuwepo kwa kutokutoa taarifa za matukio ya ukeketaji kwa Mamlaka zinazohusika kabla hata baada ya ukeketaji.

“Haiwezekani wazazi na viongozi wa vijiji na mitaa wanaoishi na hawa watoto waache watoto ambao walishakimbia kukeketwa bila ya wao kutoa taarifa kwa mamlaka zinazohusika ili kuwanusuru watoto hao au kuwachukulia hatua watu wote wanaohusika na ukeketaji” alisema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amewataka viongozi wa Serikali, Siasa, Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGOs) katika Mkoa wa Mara kujitathmini kuhusu namna wanavyosaidia au kukwamisha mapambano dhidi ya ukeketaji katika Mkoa wa Mara.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara amelaani tamko lililotolewa hivi karibuni na wazee wa mila wa koo za Wakurya kuruhusu ukeketaji kuendelea hata baada ya msimu wa kawaida wa ukeketaji kuisha na kufanya matambiko ya kuruhusu ukeketaji kuendelea katika kipindi ambacho kilizoeleka sio cha ukeketaji.

“Tamko hili la wazee wa mila linarudisha nyuma jitihada za Serikali na wadau wa maendeleo kupambana na ukatili wa kijinsia na hususan ukeketaji katika Mkoa wa Mara, hatutakubali kuwavumilia, tutawachukulia hatua wote watakaohusika” alisema Mheshimiwa Mzee. 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara Mheshimiwa Patrick Chandi Marwa ameeleza kuwa wananchi wa Mkoa wa Mara wanatakiwa kulipa umuhimu suala la kupambana na ukatili wa ukeketaji kwa wasichana na wanawake.

Amewashauri wazee kuendeleza mila nzuri zenye kuleta maendeleo ya jamii na kuacha mila mbaya kama za kukeketa wanawake kutokana na athari za mila hizo katika jamii.

“Tatizo kubwa ni kuwa mwanamke akitahiriwa anaolewa haraka, kuna umuhimu wa kutoa elimu zaidi kwa wanaume ili waache kuoa wanawake waliokeketwa na wote wanaojihusisha na ukeketaji wa wanawake ”alisema Mheshimiwa Chandi.

Mheshimiwa Chandi ameeleza kuwa wazazi wengi wanapenda watoto wao wakeketwe kwa sababu ya matumaini kuwa watoto wao wataolewa na watapata mali nyingi na hususan ng’ombe.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Kamati ya Usalama ya Wilaya za Tarime, Serengeti na Butiama, baadhi ya maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Menejimenti za Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Serengeti na Butiama.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa