• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mhe. Silinde aipongeza Tarime DC na Mji wa Bunda

Posted on: December 5th, 2022

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa Mhe. David Ernest Silinde leo amehitimisha ziara yake Mkoa wa Mara kwa kuzipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na Halmashauri ya Mji wa Bunda kwa kwa kazi nzuri ya ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Mheshimiwa Silinde ametoa pongezi hizo katika maeneo tofauti tofauti baada ya kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Akiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Mheshimiwa Silinde ametembelea Shule ya Sekondari ya Nyabisaga (madarasa 3), Shule ya Sekondari ya Nyantira (madarasa 2), na Shule ya Sekondari ya Kemambo (darasa 1) yote yakiwa katika hatua za ukamilishaji.

Mheshimiwa Silinde akiwa katika Shule ya Sekondari ya Kemambo amemtaka Afisa Elimu wa Mkoa wa Mara kutoa motisha kwa Shule ya Sekondari ya Kemambo kwa kukamilisha mapema ujenzi wa madarasa ambapo Waziri alikuta mafundi wakiendelea kufanya usafi baada ya kazi ya ujenzi kukamilika.

Katika Halmashauri ya Mji wa Tarime, Mheshimiwa Silinde ametembelea Shule ya Sekondari ya Nyamisangura ambayo awali ilipewa fedha za kujenga vyumba 11 vya madarasa, lakini baadaye vyumba vitano kati ya hivyo vilihamishiwa katika Shule ya Sekondari ya Turwa B na shule hiyo kubaki na vyumba sita vya madarasa.

Hata hivyo, vyumba vitatu vilikuwa kwenye uezekaji wakati vyumba vitatu vingine vikiwa kwenye lenta jambo ambalo halikumfurahisha Mheshimiwa Naibu Waziri.  

Naibu Waziri pia alitembelea Shule ya Sekondari ya Bunda (madarasa 3) na Shule ya Sekondari ya Nyamikokoto ambayo inajengwa mpya kupitia mradi wa SEQUIP katika Kata ya Bunda Stoo ambayo itachukua wanafunzi wa Kata ya Bunda Mji na Kata ya Bunda Stoo.

Katika ziara hiyo, Naibu Waziri aliambatana na Wakuu wa Wilaya za Tarime na Bunda, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala Wasaidizi Sehemu ya Elimu na Sehemu ya Miundombinu, Mbunge wa Tarime Vijijini, Wenyeviti na Wakurugenzi wa Halmashauri, watumishi wa Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa