• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MARA yawaomba waandishi kuelimisha jamii

Posted on: December 19th, 2023

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Dkt. Zabron Masatu leo Desemba 11, 2023 amefungua mafunzo ya Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Mara yanayofadhiliwa na Mradi wa Afya Thabiti unaotekelezwa na Shirika la AMREF Afrika na kuwataka Waandishi wa Habari kutoa elimu za mapambano dhidi ya UKIMWI.

Akizungumza wakati wa uhufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mwembeni Complex, Dkt Masatu ameeleza kuwa Waandishi wa Habari wanaomchango mkubwa sana katika kuielimisha jamii katika mapambano hayo.   

“Jamii ikujua umuhimu wa kupima afya na ikapima na kupokea majibu na ushauri wa wataalamu  inaweza kusaidia katika kupunguza maambukizi ya UKIMWI” amesema Dkt. Masatu

Dkt. Masatu ameeleza kuwa ili kufanikiwa kupunguza kasi ya maambukizi katika Mkoa wa Mara, ushirikiano baina ya Serikali, watoa huduma za afya na Waandishi wa Habari unahitajika sana ili kuweze kufikia malengo ya kupunguza maambukizi.

Aidha, Dkt. Masatu amewashukuru sana Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Mara kwa ushirikiano wanaoutoa katika kutangaza shughuli, Kampeni na miradi mbalimbali ya Sekta ya Afya.

“Dunia inalenga kuwa ifikapo mwaka 2030 kusiwepo maambukizi ya UKIMWI na hili litafanikiwa kama Waandishi wa Habari na vyombo vya Habari vitashiriki katika kuuelimisha umma kuhusu namna ya kujiepusha na maambukizi ya UKIMWI” amesema Dkt. Masatu.

Kwa upande wake Mratibu wa Upimaji UKIMWI na Tohara Kinga Mkoa wa Mara Bwana Felix Mtaki  ameeleza kuwa kiwango cha maambukizi katika Mkoa wa Mara kimepanda kutoka asilimia 3.6 miaka mitano iliyopita hadi asilimia 5 mwaka jana.

Bwana Mtaki ameeleza kuwa maambukizi hayo yameongezeka kutokana na sababu mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

“ Kiwango cha maambukizi kwa Mkoa wa Mara ni kikubwa kuliko kiwango cha kitaifa cha asilimia 4.5” amesema Bwana Mtaki na kuzitaja sababu ya ongezeko hilo kuwa ni pamoja na uwepo wa shughuli za uchimbaji wa madini, uvuvi na mila na tamaduni za wananchi wa Mkoa wa Mara.

Bwana Mtaki ameeleza kuwa baadhi ya makabila hayafanyi tohara kwa wanaume wakati kiutaalamu tohara inasaidia kuepuka maambukizi ya UKIMWI kwa asilimia 60 na hivyo jamii hizi zipo kwenye hatari ya maambukizi zaidi ya UKIMWI.

Aidha, ameitaja sababu nyingine ni kuwepo kwa mtandao wa ngono ambapo watu wengi wanakuwa na wapenzi zaidi ya mmoja na hivyo kueneza maambukizi ya virusi kwa haraka zaidi.

Wakati huo huo, Mratibu wa Kudhibiti  UKIMWI, Magonjwa ya Ngono na Homa ya Ini Mkoa wa Mara  Dkt. Omari Gamuya ameeleza kuwa Mkoa wa Mara unatekeleza mikakati mbalimbali ili kuhakikisha maambukizi mapya yanapungua katika jamii ikiwemo na kampeni za kutoa elimu katika ngazi ya jamii.

Aidha, Mkoa kwa kushirikiana na wadau umeanza kutoa huduma za dawa tiba kwa kutumia alama za vidole ambayo imesaidia kutoa dawa sahihi

Mafunzo ya Waandishi wa Habari ya siku tatu kuanzia tarehe 11 Desemba, 2023 yamehudhuriwa na Wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Shirika la AMREF Afrika na Waandishi wa Habari kutoka baadhi ya vyombo vya Habari vya Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • Waongozeni wanafunzi kufikia ndoto zao- Kusaya

    May 29, 2025
  • Kamati za Maafa Mkoa wa Mara zajengewa Uwezo

    May 26, 2025
  • Kikwete achangisha milioni 200 za ujenzi wa kanisa Mara

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa