• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara Yaishukuru Serikali kwa miradi ya Kimkakati

Posted on: April 23rd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 23 Aprili, 2025 ameshiriki ziara ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika ikiwa ni sehemu ya sherehe za miaka 61 ya Muungano katika Mkoa wa Mara ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha za kutekeleza miradi ya kimkakati katika Mkoa wa Mara.

Mhe. Mtambi ametoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti wakati Katibu Mkuu wa CCM alipokuwa anakagua miradi ya Uwanja wa Ndege Musoma na Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (Kwangwa).

“Mhe. Rais amekuwa akiutazama Mkoa wa Mara kwa namna ya kipekee sana na amekuwa akileta fedha za kutekeleza miradi mingi ya kimkakati ambayo itachechemua maendeleo ya Mkoa na Nchi ya Tanzania” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema Serikali ya Awamu ya Sita imeleta fedha za kutekeleza miradi ya kimkakati katika sekta zote na imebadilisha mwelekeo wa maendeleo ya Mkoa kwa kiasi kikubwa sana.

Mhe. Mtambi amewaomba wananchi wa Mkoa wa Mara kumshukuru Rais na Serikali kali yake kwa vitendo na hususan kwa kuiunga mkono juhudi Serikali katika kuwaletea maendeleo na kuwakumbuka msemo kuwa “akufaae kwa dhiki ndio rafiki wa kweli”.

Mhe. Mtambi ametolea mfano Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ni Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya kwanza ya Serikali katika mikoa ya Kanda ya Ziwa na inahudumia wagonjwa kutoka Mkoa wa Mara, Mikoa jirani na nchi jirani.

“Hili jengo ni kubwa sana japokuwa ujenzi wake ulianza zamani lakini jengo hili linauwezo wa helikopta kutua juu yake na mgonjwa kupokelewa hapa hapa hospitalini” amesema Mhe. Mtambi.

Kwa upande wake, Mbunge wa Musoma Mhe. Vedastus Mathayo amesema wananchi wa Mkoa wa Mara wameufuatilia ujenzi wa uwanja wa Ndege Musoma kwa muda mrefu na sasa unaenda kuanza kutoa huduma kuanzia Septemba, 2025.

Mhe. Mathayo amemuomba Mhe. Nchimbi kufuatilia fidia ya zaidi ya shilingi bilioni 5.2 wanaodai wananchi watakaopisha mradi wa ujenzi wa jengo la abiria katika uwanja huo madai ambayo yametoka kwa Mthamini Mkuu wa Serikali kwenda Hazina kwa ajili ya malipo.

Mhe. Mathayo ameipongeza Serikali kwa miradi mingi inayoendelea kutekelezwa katika Wilaya ya Musoma ambayo amesema imebadilisha utoaji wa huduma kwa wananchi wa Manispaa ya Musoma na maeneo ya jirani.

Baada ya hapo, Ziara ya Mhe. Nchimbi iliendelea ofisi za Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara ambapo amekagua mradi wa ukumbi na kufanya kikao na Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa iliyoboreshwa.

Kesho ziara ya Katibu Mkuu wa CCM inaendelea katika Wilaya ya Butiama ambapo anatarajia kutembelea Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere cha Kilimo na Teknolojia (MJUNUAT) Butiama, kaburi la Baba wa Taifa na kufanya mkutano wa hadhara katika eneo la Kiabakari.

Katika ziara hiyo, Mhe. Nchimbi ameambatana na viongozi na Watendaji wa CCM na Serikali na kauli mbiu ya miaka 61 ya Muungano ni “Muungano wetu ni Dhamana, heshima na tunu ya Taifa, Shiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025”.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Kusaya apokea vifaa vya mapambano dhidi ya HIV/UKIMWI

    May 06, 2025
  • Mtambi ataka elimu zaidi kutunza Maeneo ya Urithi wa Dunia

    May 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa